inspire

inspire

Lebo

AFYA (8) AJIRA (5) BIASHARA (39) ELIMU (14) MAHUSIANO (2) MALEZI (16) MAZINGIRA (12) SAIKOLOJIA (48) VIJANA (7)

Business registration

Green Consulting

business consultancy

business consultancy

Business consulting-2

Business consulting-2

Professional Consulting

PDC

Swahili translator

Swahili translator

TANGAZO-KITABU

E-BOOK: MTAZAMO WAKO NI UPI?

TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- .... TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- ....

TANGAZO TUWEZESHANE

TANGAZO TUWEZESHANE

DARDY'S INVST-20/10/2017

DUNIA IKUONE

DUNIA IKUONE

Jumatatu, 26 Agosti 2013

BIASHARA: UKITAKA KUJENGA BIASHARA IMARA NA YENYE MAFANIKIO FANYA HIVI…



Kumekuwepo na changamoto nyingi kwa wafanyabiashara wadogo pia hata wale wanaolekea kuwa na biashara kubwa.Moja ya changamoto kubwa kwa biashara ndogo na zilizoanza ni kushindwa kukuza soko la biashara na faida ndogo iliyo tofauti na malengo ya mmliki/wamiliki wa biashara fulani.Pia mitaji midogo ni changamoto nyingine inayodidimiza kupanuka kwa biashara ndogo.
Tukitambua na kuzitumia changamoto zilizopo kama sehemu ya kusimamia ni vyema tukashirikishana kwa pamoja mbinu 10 mbadala za kuboresha biashara zetu kwa mafanikio tarajiwa kwa muda tuliojipangia.

1.ANDIKA NA UFUATE MPANGO WA BIASHARA “Business plan”
Ukiwa na wazo la biashara ni vyema ukafanya upembuzi yakinifu kupitia mpango wako wa biashara.Kupitia mpango huo wa biashara uliouandika utaweza kupunguza hatari zilizopo katika biashara yako,pia utaona ni kwa njia ipi utapata faida na utajua muelekeo wa biashara yako kuliko kuingia kichwa kichwa katika biashara.
2.PENDA KILE UNACHOKIFANYA, utakifanya kwa bidii…Kama Steve Jobs- mjasiriamali, mwanzilishi na mkurugenzi mtendaji wa Kampuni ya "Apple Computers na Pixar Animation" alivyosema; “huna sababu ya kutofuata ukipendacho” Hii ni muhimu sana kwa biashara changa.
3.IFANYE BIASHARA YAKO KUWA NA HUDUMA AU BIDHAA ZA KIPEKEE
Kufanikisha hili fanya utafiti wa soko la bidhaa na huduma za washindani wako, BORESHA! ukijitofautisha nao ila ukihakikisha unakidhi mahitaji ya wateja wako.
4.HAKIKISHA UNAWASHIKA WATEJA WAKO…fanya hivi ukichukulia kama wamekuja ofisini kwako kwa mara ya kwanza…usiwachukulie kimazoea na kuwapuuza.Hili ni muhimu sana kwa wateja wa mwanzo kwa sababu wanakwenda kukufanyia matangazo bila gharama yeyote.
5.TENGENEZA WIGO WA SOKO LAKO
Hakikisha unalenga wahusika wa aina fulani.Mfano.Kama unauza nguo za jaribu kujitofautisha na wengine kwa kuzingatia rika na jinsia.Hii itakusaidia kuitofautisha biashara yako na wengine hivyo kuwa na wigo wa uhakika wa soko lako kibiashara.
6.JITENGENEZEE MTANDAO MZURI…zingatia ushirikiano wa kibiashara wenye kufaidiana kibidhaa au kihuduma.Mfano kampuni moja haiwezi kuwa na kila kitu, ni lazima itahitaji huduma au bidhaa kutoka kampuni nyingine…hii nisehemu nzuri ya kutenga mtandao mzuri ukiwa makini kuangalia fursa.
7.WEKA LENGO LA KUIFANYA BIASHARA YAKO KUKUA IKIWA NA FAIDA ENDELEVU…
Tukizingatia ushauri wa wafanyabiashara…inatambulika kuwabiashara imara na yenye tija ya faida endelevu ni ile inayokuwa kulingana na muda na malengo ya kukua.Inatarajiwa kuwa biashara iliyokuwa inahusisha kutembeza bidhaa inaweza kuonyesha hali ya kukua hasa kwa kumiliki duka la bidhaa.
8.SOMA ALAMA ZA NYAKATI
Ni vyema kujua aina na wakati wanapopatika wateja wako kulingana na aina ya bidhaa au huduma yako. Usifanye biashara kimazoea ukiwa na lengo la kukuza biashara yako.Hakikisha unabadilika kulingana na mazingira…na hii ni sifa mojawapo ya mjasiriamali.
9.THAMINI NGUVU YA TEKNOLOJIA YA HABARI NA MAWASILIANO
10.USIKATE TAMAA PALE UNAPOPATA HASARA...tumia mapungufu yako kujiboresha zaidi.
Imetolewa na
Jielimishe Kwanza!