inspire

inspire

Lebo

AFYA (8) AJIRA (5) BIASHARA (39) ELIMU (14) MAHUSIANO (2) MALEZI (16) MAZINGIRA (12) SAIKOLOJIA (48) VIJANA (7)

Business registration

Green Consulting

business consultancy

business consultancy

Business consulting-2

Business consulting-2

Professional Consulting

PDC

Swahili translator

Swahili translator

TANGAZO-KITABU

E-BOOK: MTAZAMO WAKO NI UPI?

TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- .... TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- ....

TANGAZO TUWEZESHANE

TANGAZO TUWEZESHANE

DARDY'S INVST-20/10/2017

DUNIA IKUONE

DUNIA IKUONE

Ijumaa, 13 Septemba 2013

MJASIRIAMALI: WANAOKUPINGA, KUKUDHARAU,KUKUWEKEA VIKWAZO NA KUKUKEJELI WANAKUJENGA BILA WEWE NA WAO KUJIJUA…

-->
Najua jinsi inavyouma au kukatisha tamaa unapokuwa na wazo lako la biashara unaloliamini sana kukutoa kimaisha. Imezoeleka sana kwa watu kupenda kuwashirikisha ndugu, marafiki au jamaa wa karibu malengo yao ya biashara.Yafuatayo ni baadhi ya majibu wanayopata wajasiriamali wachanga mara tu baada ya kueleza nia zao za kuanzisha biashara;

·      Mh! Yalimshinda…………utaweza wewe?

·      Hivi nani kakwambia biashara hiyo inalipa kwa sasa!

·      Huogopi kupata hasara? Wengi sana wameporomoka na hiyo biashara!

·      Hiyo biashara inahitaji mtaji mkubwa sana, hakika hutaimudu!

·      Utapata wapi mtaji?

·      Hebu acha kupoteza muda wako…

Bila shaka maswali haya yanakatisha tamaa na kukupa hasira.Naomba nikufumbue macho ndugu msomaji…hasira hiyo ndiyo inayokufanya uboreshe sehemu zote zenye mapungufu katika wazo lako la biashara.

Hivyo, hupaswi kugombana wala kurumbana na kundi hilo linalokupa changamoto.Suala la msingi ni kutulia, kushusha pumzi, hasira zetu na kuwasikiliza kwa makini na kuwa wajanja kung’amua sehemu zenye mapungufu na kuboresha.

Faida nyingine ya kundi hilo linalotoa changamoto ni kukupa msukumo wa kusonga mbele na kukupa hasira ya kumiliki vitu binafsi.
Jaribu kufanya utafiti mwenyewe utakubaliana nami na hata kuamua kunipigia simu +255 754 572 143.
Ukiona watu wanakupongeza na kukubali kila unachowaambia…kuna walakini!

“I like oppositions and criticism ,they make me behave better with perfection-Henry Kazula.
USIOGOPE VIKWAZO, KUPINGWA...CHUKULIA HALI HIYO KAMA SEHEMU YA KUJIJENGA ZAIDI, UKIBORESHA UTENDAJI WAKO!
Imetolewa na
Jielimishe Kwanza!


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni