inspire

inspire

Lebo

AFYA (8) AJIRA (5) BIASHARA (39) ELIMU (14) MAHUSIANO (2) MALEZI (16) MAZINGIRA (12) SAIKOLOJIA (48) VIJANA (7)

Business registration

Green Consulting

business consultancy

business consultancy

Business consulting-2

Business consulting-2

Professional Consulting

PDC

Swahili translator

Swahili translator

TANGAZO-KITABU

E-BOOK: MTAZAMO WAKO NI UPI?

TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- .... TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- ....

TANGAZO TUWEZESHANE

TANGAZO TUWEZESHANE

DARDY'S INVST-20/10/2017

DUNIA IKUONE

DUNIA IKUONE

Alhamisi, 5 Septemba 2013

MTAZAMO: TUNZA RASILIMALI MUDA KWA MANUFAA!

-->
Picha na www.empowernetwork.com
Kumekuwa na mazoea kwa jamii za watu wengi hasa nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara kuchukulia suala la kutunza rasimali muda kama mzaha au kitu fulani cha kuchezea na kupuuzia. Hili ni tatizo, lazima tukubaliane kutokukubalina! ili kubadili mtazamo uliopo.
Nilipoanza kujifunza jinsi ya kutunza muda kupitia watu wanaotunza muda na kujisomea vitabu mbali mbali niligundua siri kubwa katika utunzaji rasilimali muda.Kwa sasa naweza kufanya mambo mengi katika ratiba niliyojiwekea.Nimetenga muda maalum pia kukuandikia ndugu msomaji ili nawe upate kupona na ugonjwa huu ambao unaonekana ni wa kawaida ilihali unateketeza uchumi wa mtu mmoja na taifa kwa ujumla.

Ifahamike kuwa muda ni rasimali kama rasimali nyingine mfano madini…endapo utatumika vibaya ni dhahili kabisa tutarudi kwenye ule usemi usemao “majuto ni mjukuu.”

Nikichukulia mfano jijini Dar es salaam nchini Tanzania, utakutana na watu wenye visingizio kadha wa kadha kuhusiana na utunzaji wa muda…wengi wamekuwa wakichelewa kuripoti kazini na kusababisha huduma nyingi kutotolewa kwa wakati, kubwa likiwa foleni barabarani.

Unaweza kuweka ahadi na mtu akiwa yeye ndiye alipendekeza muda na siku wa kukutana, chakushangaza anakuwa wa kwanza kuchelewa kufika eneo la ahadi na kuanza kutoa visingizio.

Pia kuna makundi ya watu wengine wajulikanao kama wapoteza muda…wanajisifu kabisa kwa kusema; ah! tupo hapa tu tunapoteza poteza muda.” Wengine wanatumia muda vibaya kwa kupiga soga na kusengenya wengine.

Tunaweza kuhama hapo kwa  kufuata na kufanya mambo 10 yafuatayo:

1. JIWEKEE MPANGO WA SIKU WENYE MANUFAA UNAOWEZA KUUTEKELEZA KWA WAKATI HUSIKA


2.  TAMBUA KUWA RATIBA YA KESHO HAIPANGWI KESHO ASUBUHI…INAPANGWA KABLA YA KULALA

3.  TUMIA SIMU YAKO KUKUKUMBUSHA MAJUKUMU YA SIKU NA MUDA HUSIKA

4.  UNAPOWEKA AHADI NA MTU HAKIKISHA UMETATHIMINI MUDA UTAKAOTUMIKA UKIWA NJIANI…UTAEPUKA KUSINGIZIA FOLENI

5.   JIJENGEE HALI YA UAMINIFU KATIKA KUTIMIZA AHADI KWA WAKATI

6.    JIJENGEE TABIA KUSOMA VITABU VYENYE MANUFAA ILI KUEPUKANA NA KUPIGA SOGA

7.    THAMINI MUDA WA WENGINE…TAMBUA KUWA WANA MAJUKUMU

8. TAMBUA KUWA UNAPOHARIBU RATIBA YA MTU MMOJA UMESABABISHA WATU WENGINE WENGI KUHARIBU RATIBA ZAO

9.     KUWA MTU WA MFANO KUJALI MUDA MARA KWA MARA, WENGINE WATAKUIGA

10. USIAMINI SANA KUHUSU DHARULA…EPUKA KUHAIRISHA HAIRISHA MAMBO YALIYOPANGWA

Nakutakia mafanikio mema katika kuwa mtu wa kutunza rasilimali muda kwa manufaa yako na wengine.

Imetolewa na
Jielimishe Kwanza!

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni