inspire

inspire

Lebo

AFYA (8) AJIRA (5) BIASHARA (39) ELIMU (14) MAHUSIANO (2) MALEZI (16) MAZINGIRA (12) SAIKOLOJIA (48) VIJANA (7)

Business registration

Green Consulting

business consultancy

business consultancy

Business consulting-2

Business consulting-2

Professional Consulting

PDC

Swahili translator

Swahili translator

TANGAZO-KITABU

E-BOOK: MTAZAMO WAKO NI UPI?

TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- .... TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- ....

TANGAZO TUWEZESHANE

TANGAZO TUWEZESHANE

DARDY'S INVST-20/10/2017

DUNIA IKUONE

DUNIA IKUONE

Jumatano, 4 Desemba 2013

AJIRA: ATHARI YA KUFANYA KAZI KATIKA MAZINGIRA YA UTUMWA WA KISASA KWA MFANYAKAZI"


N
ikirejea makala zangu mbili kuhusu kazi na ajira: jielimishekwanza.blogspot.com/2013/10/ajira-na-kazi-jiepushe-zuia-utumwa-wa.html na http://jielimishekwanza.blogspot.com/2013/10/kazi-na-ajira-hivi-ni-viashiria-vya.html nataka nikujuze kuhusu athari kwa mfanyakazi aliye katika mfumo wa kazi wenye chembe chembe za Utumwa wa Kisasa kama ijulikanavyo kwa lugha ya Kiingereza (Modern-day Slavery).
 
Kutokana na utafiti wa hivi karibuni uliofanywa na Jielimishe Kwanza! katika maeneo mbali mbali ya kazi, umebaini  athari zifuatazo, ambazo huwapata wafanyakazi katika mazingira ya kazi;

1.Kushuka kwa hamasa na shauku ya kufanya kazi.Hivyo, wafanyakazi wengi wanafanya kazi kwa mazoea tu, bora siku ziende.

2.Kudhoofika kwa ubunifu na mbinu za utendaji wa mfanyakazi binafsi…mfanyakazi anakuwa na mtu wa kufuata maelekezo tu!

3.Kuongezeka kwa manung’uniko ya chini chini na migomo baridi kazini.

4.Kufanya kazi kwa hofu ya kukosa ajira…hapa ndipo uhuru wa mfanyakazi unapotekwa. Soma makala inatakayofuata: “Hivi ndivyo uhuru wako unavyoweza kutekwa”.

5.Kukosa fursa ya kuchangia na kutoa maoni katika kuboresha maslahi ya mfanyakazi…maamuzi ya uongozi ni ya mwisho haijalishi mfanyakazi ana mchango gani kwenye kampuni, shirika au taasisi.

Ikiwa unakumbwa na athari mojawapo kati ya hizi, jichunguze kwa makini, je una mchango gani katika eneo la kazi? Nini kinahitajika kazini ili uweze kuheshimiwa na kupata haki yako kulingana na jitihada zako?...ukiwa huna jibu sahihi au upo njia panda usisite kuwasiliana na jopo la Jielimishe Kwanza! katika eneo husika, utapata ufumbuzi wa kuishi kwa ndoto yako na kufuata kile moyo unapenda kufanya.
Tunakutakia kila la heri katika kupambana na utumwa wa kisasa katika maeneo ya kazi.
Imetayarishwa na kutolewa na
Jielimishe Kwanza!

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni