inspire

inspire

Lebo

AFYA (8) AJIRA (5) BIASHARA (39) ELIMU (14) MAHUSIANO (2) MALEZI (16) MAZINGIRA (12) SAIKOLOJIA (48) VIJANA (7)

Business registration

Green Consulting

business consultancy

business consultancy

Business consulting-2

Business consulting-2

Professional Consulting

PDC

Swahili translator

Swahili translator

TANGAZO-KITABU

E-BOOK: MTAZAMO WAKO NI UPI?

TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- .... TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- ....

TANGAZO TUWEZESHANE

TANGAZO TUWEZESHANE

DARDY'S INVST-20/10/2017

DUNIA IKUONE

DUNIA IKUONE

Jumapili, 22 Desemba 2013

MTAZAMO: KUELEKEA MWAKA 2014, TUJIELIMISHE! TUJIFUNZE! TUJIPANGE UPYA KUPITIA MAKOSA…



K
ujifunza kwa kweli na kwenye tija ni kupitia MAKOSA yaliyofanyika awali, hii ni kwa sababu, hayo ndiyo yametufikisha hapa tulipo.
Nikiwa katika mapumziko, sehemu tulivu yenye upepo mwanana pembezoni mwa Mlima mrefu Afrika, uliopo nchini Tanzania-Mlima Kilimanjaro (http://www.tanzaniaparks.com/kili.html), nafakari kuhusu mwaka 2013 na kupanga mikakati kuelekea mwaka 2014…naamua kuperuzi katika maktaba yangu ndani ya “laptop” nakutana na kijitabu kiitwacho “Tujisahihishe” cha Mwl.J.K.Nyerere (1962) chenye kurasa 8.
Nikashawishika na jina la kijitabu hicho, hivyo nikataka kujua kulikoni ndani yake…Mwanzoni ilibaki kidogo niachane nacho, kwa sababu kilikuwa kikielezea makosa ndani ya T.A.N.U, najua hata wewe unaweza kusema nani anasoma vitabu vya T.A.N.U hadi leo?
Nikakumbuka msemo huu; ya kale ni dhahabu, ikanijia shauku ya kutaka kuyajua makosa hayo…yawezekana yamekufikisha/yametufikisha hapa tulipo.Nikaanza kusoma kwa makini na kufumbuka macho kujionea makosa ya mwaka 1962 ambayo Watanzania tunaendelea kuyafanya kwa kujua, kwa mazoea au kutojua…
“Nitanukuu moja ya makosa yaliyoainishwa na Mwalimu, Jielimishe Kwanza! inaliona kosa hili kubeba makosa mengine tunayoyafanya kila siku;
Kosa jingine ni kutojielimisha.Kanuni yetu ni moja inasema: “Nitajielimisha kwa kadiri ya uwezo wangu wote na kutumia elimu yangu kwa faida ya wote”. Kwa ufafanuzi zaidi, anasema; Kujielimisha siyo maana yake kwenda shuleni. Kujielimisha ni kutafuta ukweli wa mambo. Kwenda shule hutusaidia.Lakini japo hatuwezi kwenda shule twaweza kujifunza”.
Watu wengi hukoma kujielimisha mara tu wakihitimu masomo yao na kufikiri kuwa wanajua kila kitu.Mwl.J.K.Nyerere katika kitabu hicho anawaainisha:
 “watu walio hatari sana ni wale ambao wanafikiri kuwa wanajua kila kitu wala hawana haja kujifunza zaidi.
Nabainisha haya kwa kukuhamasisha ndugu msomaji kukaa chini na kutafakari makosa uliyoyafanya mwaka 2013 ili usiyarudie mwaka 2014.
Ikiwa unajiona hukufanya kosa au makosa, tambua kuwa hakuna mkamilifu katika dunia hii…Maandiko Matakatifu yamebainisha.Nilihamasika sana na mwisho wa kitabu cha Mwalimu, aliweka wazi, nanukuu; sitaki Mtu ye yote afikiri kuwa mimi niliyeandika maneno hayo sinayo makosa.Hivyo si kweli.Hii na kwangu kadhalika, najifunza sana kupitia makosa ninayofanya.
Naomba nisiwe msimuliaji sana wa maneno ya Mwalimu, hamasika kujisomea mwenyewe kijitabu hicho ili ujue makosa mengine ili yasijirudie kwako.
Tena na tena, naomba utumie wakati huu mzuri wa mapumziko kujichunguza mapungufu yako yaliyopelekea kufanya makosa uyajuayo.Jielimishe! Jipange upya kwa kujiwekea mikakati ukijifunza kwa makosa.
Nakutakia mapumziko mema na kukutakia heri na fanaka ya Krismasi na Mwaka mpya 2014.
Imetayarishwa na
Henry Kazula,
Mkurugenzi mtendaji.
Jielimishe Kwanza!

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni