inspire

inspire

Lebo

AFYA (8) AJIRA (5) BIASHARA (39) ELIMU (14) MAHUSIANO (2) MALEZI (16) MAZINGIRA (12) SAIKOLOJIA (48) VIJANA (7)

Business registration

Green Consulting

business consultancy

business consultancy

Business consulting-2

Business consulting-2

Professional Consulting

PDC

Swahili translator

Swahili translator

TANGAZO-KITABU

E-BOOK: MTAZAMO WAKO NI UPI?

TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- .... TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- ....

TANGAZO TUWEZESHANE

TANGAZO TUWEZESHANE

DARDY'S INVST-20/10/2017

DUNIA IKUONE

DUNIA IKUONE

Jumatano, 18 Desemba 2013

MTAZAMO: MAKOSA 10 YANAYOWEZA KUINYIMA AKILI YAKO UHURU WA KUFANYA KAZI YAKE BARABARA...

-->
T
 ukikumbushana moja ya makala zetu kuhusu viashiria vya kutekwa kwa uhuru wa fikra,mtazamo, uchumi wa mtu binafsi http://jielimishekwanza.blogspot.com/2013/12/mtazamo-hivi-ndivyo-uhuru-wako.html
Picha na stepontoliquid.wordpress.com
naomba nikulete kwenye makala ya  leo kuhusu makosa yanayoweza kuinyima akili uhuru wa kufanya kazi yake barabara-(mbele ya kila kosa kuna suluhisho);
1.   Kutojielimisha-kujielimisha ni njia ya kujua ukweli wa mambo
2.  Kupuuza usomaji wa makala na vitabu- ukweli wa mambo hufahamika kupitia kulinganisha mawazo ya watu tofauti tofauti…Unasoma mawazo yao kupitia vitabu au makala zao au kuongea nao.
3.   Kupuuza mawazo ya wengine-kuwa msikivu zaidi na si muongeaji zaidi bila kupuuza wazo la mwingine
4.   Kujifanya mjuaji wa yote-tambua kuwa siku zote tunajifunza vitu vipya, huwezi kujua kila kitu
5. Kuwa na majibu rahisi kwa maswali magumu(huu ni uvivu wa kufikiri)-tuepuke kubashiri kwa hisia na kutoa majibu rahisi ya matatizo/maswali magumu…tuiruhusu akili yetu itafakari kwa kujiuliza maswali ya msingi na kutoa majibu ya matatizo.
6. Kuchagua viongozi wasio na sifa…hawa hukunyima fursa ya kutoa mawazo yako na kukufanya uwe mtumwa wa fikra zao-tuwapime viongozi kwa uwezo wao wa kuongoza wenye kujua wameteuliwa kwa manufaa ya wananchi na si unafsi.Tuwaepuke viongozi wanaoamini zaidi mawazo yao binafsi kwa manufaa yao na kuyafanya ya wengi.
7.   Kutumia pombe na madawa ya kulevya kupindukia-punguza au acha matumizi ya pombe na madawa ya kulevya.
8. Kutopata muda wa kukaa mwenyewe na kutafakari maisha yako-jiwekee utaratibu wa kukaa mwenyewe na kutafakari kuhusu changamoto za maisha.
9. Kutegemea wengine wakuamulie kila kitu au wakuthibitishie maamuzi yako-jiamini, tambua kuwa wazo lako ni wewe unayejua hatma yake.Ujue kuwa katika dunia hii kuwa wakatisha tama wengi.Wakati mwingine ni vyema kufanya mambo yatokee…ukikosea, jifunze tena kwa kupitia makosa hayo.
10. Hofu ya kukosea-Wavumbuzi wengi duniani walifanya makosa mengi sana…wakajifunza kupitia makosa.(Ungana nasi kwenye makala ijayo yenye kichwa:TUJIELIMISHE! TUJIFUNZE! TUJIPANGE UPYA KUPITIA MAKOSA…
Mfano wa Thomas Edison katika kuvumbua taa ya umeme alifanya makosa 1,000.Edison alichulia makosa haya kama ni njia 1,000 za kutengeneza taa ya umeme.Jifunze kwa watu mashuhuri duniani waliofanya makosa kupitia http://www.uky.edu/~eushe2/Pajares/OnFailingG.html 
Ikiwa hujanielewa na unahitaji ufafanuzi zaidi, tafadhali usisite kuwasiliana nasi.
Imetayarishwa na kutolewa na,
Jielimishe Kwanza!  


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni