inspire

inspire

Lebo

AFYA (8) AJIRA (5) BIASHARA (39) ELIMU (14) MAHUSIANO (2) MALEZI (16) MAZINGIRA (12) SAIKOLOJIA (48) VIJANA (7)

Business registration

Green Consulting

business consultancy

business consultancy

Business consulting-2

Business consulting-2

Professional Consulting

PDC

Swahili translator

Swahili translator

TANGAZO-KITABU

E-BOOK: MTAZAMO WAKO NI UPI?

TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- .... TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- ....

TANGAZO TUWEZESHANE

TANGAZO TUWEZESHANE

DARDY'S INVST-20/10/2017

DUNIA IKUONE

DUNIA IKUONE

Jumanne, 14 Januari 2014

MTAZAMO 2: HIVI NDIVYO UNAVYOWEZA KUTUMIA MTAZAMO WA WENGINE KUKUHUSU WEWE NA KUJIONGEZEA UTHAMANI…

-->

It’s what we learn about ourselves from our response that really matters-Marissa Walter
________________________________________________________________________________________

N
dugu msomaji, najua unaambatana nami kuhusiana na makala iliyopita kuhusu unavyojiona, unavyowaona na vile wanavyokuona wengine.http://jielimishekwanza.blogspot.com/2014/01/mtazamo-unavyojiona-unavyowaona-na-vile.html
Kama nilivyoeleza katika makala hiyo kuwa, kuna utofauti wa kimtazamo kwa sisi tunavyojiona ukilinganisha na ule wa wengine.
Moja kwa moja nikulete kwenye jinsi unavyoweza kutumia mtazamo wa wengine kukuhusu wewe na kujiongezea uthamani katika utendaji kazi na maisha ya kila siku.
Zipo njia mbali mbali zitakazokufanya uweze kutumia mtazamo wa wengine kujiongezea uthamani, nitainisha njia tano (5) zinazobeba nyingine;
1.Jitambue uwezo wako wa asili kabla ya wengine hawajakueleza.Hii ni njia muhimu sana…inatengeneza sehemu ya kuanzia kupima mtazamo wako kiutendaji.(Hili huanza na shauku au hamasa iliyo sanjali na uwezo wako wa ndani).
2.Kuwa mwepesi kupokea mawazo kutoka kwa wengine kutokana na mitazamo yao kukuhusu(uwe makini kulinganisha mawazo yako na yao ukisimamia sifa zinazoendana na wewe).
3.Usichukulie kama unadharaulika kutokana na mitazamo ya wengine kuhusu uwezo wako wa ndani…chukulia changamoto wanazozileta kama njia ya kuboresha mapungufu uliyonayo katika utendaji wako.(Tambua kuwa kuna watu wengine wapo kukukatisha tamaa, hawakutakii mema…utawajua kwa kusikiliza mawazo yao ukilinganisha na uwezo wako na mawazo ya wengi kukuhusu wewe).
4.Watumie vizuri watu unaofanana nao mtazamo…hawa watakuimarisha zaidi.
5.Usishawishike kubadisha mtazamo wako kuhusu ulivyo na utendaji kila wakati…hii itakufanya usiwe na msimamo, mwisho wa siku hautakuwa na kitu cha kusimamia na kutambulisha uwezo wako wa asili.Mfano:Ukiwa na shauku ya kuwa mwana mageuzi,kiongozi halafu mtu mwingine akakueleza kuwa huna sifa/karba hiyo na una sifa nyingine tofauti ilihali wengi wanathamini uwezo wako.
Picha na
--> ferociousstrength.com

Lakini mwisho wa siku, cha muhimu zaidi ni vile unavyojiona mbele ya watu wengine.Maoni yao kukuhusu wewe yanaongezea na kujenga uwezo wako kwa njia moja au nyingine kama utayachukulia kwa mtazamo chanya.
Nakutakia kila la heri katika kutumia mtazamo wako na wa wengine katika kuboresha uthamani wako.
Imetayarishwa na kutolewa na 
Henry Kazula
Jielimishe Kwanza!

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni