inspire

inspire

Lebo

AFYA (8) AJIRA (5) BIASHARA (39) ELIMU (14) MAHUSIANO (2) MALEZI (16) MAZINGIRA (12) SAIKOLOJIA (48) VIJANA (7)

Business registration

Green Consulting

business consultancy

business consultancy

Business consulting-2

Business consulting-2

Professional Consulting

PDC

Swahili translator

Swahili translator

TANGAZO-KITABU

E-BOOK: MTAZAMO WAKO NI UPI?

TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- .... TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- ....

TANGAZO TUWEZESHANE

TANGAZO TUWEZESHANE

DARDY'S INVST-20/10/2017

DUNIA IKUONE

DUNIA IKUONE

Jumamosi, 25 Januari 2014

MTAZAMO: MAMBO TUNAYOSOMA, KUSIKILIZA NA KUTAZAMA YANATUJENGA KITABIA



K
atika maisha yetu ya kila siku tunakutana na mambo mbali mbali, mambo hayo tunayoyaona,kusoma na kusikiliza yana mchango mkubwa katika kujenga tabia zetu kwa njia moja au nyingine.
Mambo yote hayo yanaweza kutujenga na kuonyesha tabia hasi au chanya mbele ya jamii kulingana na mazingira.
Nikimnukuu msanii wa muziki wa kufoka foka nchini Tanzania, Farid Kubanga almaalufu kama 
Fid Q katika wimbo wake wa Propaganda kuna mstari anaimba-“tunajenga tabia kisha tabia zinatujenga” …hii ni kweli kabisa, tabia tunazozijenga kutokana na mazoea mbali mbali kwa kujua au kutokujua, zinatujenga kitabia.
Ijulikane kuwa,tabia ikijijenga ni vigumu kuibadili, ukweli huu ni sawa alivyoimba msanii wa muziki wa mashairi ya kughani Mrisho Mpoto katika wimbo wake wa “Nikipata nauli” kuwa, tabia ni kama ngozi ya mwili hauwezi kuibadili…ni afadhali iwe njema, ikiwa mbaya ni hatari kwa mtu binafsi na Taifa kwa ujumla.
Ikiwa unasikiliza,kusoma au kutazama masuala yenye mtazamo hasi na yenye hali ya hofu ya kutothubutu, ni hakika kabisa kuwa utakuwa ni mtu wa mashaka katika maisha yako.
Pia kuna masuala yanayovuta hisia na faida yake ni kitambo kidogo, haya yote kwa namna moja au nyingine yanajenga tabia ya msomaji,mtazamaji au msikilizaji na hatimaye kupelekea kuonyesha tabia hizo kwa vitendo mbele ya jamii.
Kwa hakika, tabia zetu na matendo yetu ni mazao ya masuala mbali mbali tunayoyasoma,kuyasikia na kuyaona.Hii hutokea pale tu tunapoamua kujifunza na kuyaweka katika utekelezaji kwa mazoea na hatimaye kuwa tabia.Unaweza usiamini haya niyasemayo, kwa sababu yanatokea kwetu bila kujijua…hadi mtu mwingine mwenye kujua tabia za watu atueleze.
Nikitoa mfano mdogo tu wa tabia ya ukatili kwa binadamu wenzetu, hii hutokea kwa mtu kuwa na mazoea ya kusoma,kusikiliza,kutazama sinema/video za watu makatili.Utaniuliza inawezekanaje mazoea yakasababisha mtu kuwa katili kwa wengine? Hii hutokea kwa sababu ya kuchukulia matendo ya watu makatili tunaowaona,kuwasikiliza na kusoma taarifa zao kimazoea katika maisha ya kawaida.Filamu mbali mbali za kikatili huwaaminisha watu kuwa matendo yaonekanayo ni ya kawaida tu ilhali si kweli.
Mfano mwingine ni ule wenye kuchochea tabia njema na yenye maendeleo na kupelekea mtu kubadilika kitabia kutokana na kusoma vitabu vyenye kuonyesha mbinu za mafanikio pia kuangalia filamu zenye kuchochea maarifa na utendaji bora wa kazi, hivyo kuleta maendeleo kwa mtu husika na taifa kwa ujumla.Fuatilia historia ya mafanikio ya watu mashuhuri duniani utagundua ukweli wa jambo hili.
Kufikia hapa unaweza kujichunguza mwenyewe, unapendelea kusoma,kusikiliza,kutazama mambo gani? Je, yana tija ya kukukomboa kiuchumi au yanakufanya uwe msindikizaji ya mafanikio ya wengine? Au yanakupa hofu ya kuchukua hatua ya kuthubutu kuelekea katika safari ya mafanikio? Sambamba na hilo, je unatumia muda katika njia ya kuzalisha faida au hasara? Majibu unayo mwenyewe…Tumia muda huu kuchagua kusoma,kusikiliza au kutazama mambo yanayojenga tabia njema, amini usiamini hutakuwa vile ulivyo sasa.
Nakutakia kila la heri  katika kujiepusha na mambo yasiyojenga tabia njema na kukutisha na kukukatisha tama ya kusonga mbele kimaendeleo…soma,angalia,sikiliza mambo yenye kuchochea mtazamo chanya…utapata ujasiri wa kuleta mabadiliko yenye tija ya maendeleo binafsi na  nchi yako kwa ujumla.
Imetayarishwa na kutolewa na
Jielimishe Kwanza! 

Kwa udhamini wa ………………………………..(bofya hapa kuwa mdhamini na ujitangaze zaidi).



Hakuna maoni:

Chapisha Maoni