inspire

inspire

Lebo

AFYA (8) AJIRA (5) BIASHARA (39) ELIMU (14) MAHUSIANO (2) MALEZI (16) MAZINGIRA (12) SAIKOLOJIA (48) VIJANA (7)

Business registration

Green Consulting

business consultancy

business consultancy

Business consulting-2

Business consulting-2

Professional Consulting

PDC

Swahili translator

Swahili translator

TANGAZO-KITABU

E-BOOK: MTAZAMO WAKO NI UPI?

TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- .... TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- ....

TANGAZO TUWEZESHANE

TANGAZO TUWEZESHANE

DARDY'S INVST-20/10/2017

DUNIA IKUONE

DUNIA IKUONE

Jumapili, 9 Machi 2014

BIASHARA: NJIA PEKEE ZA KUPAMBANA NA KUMSHINDA MSHINDANI WAKO KATIKA BIASHARA…(SEHEMU 2)




Huu ni muendelezo wa makala iliyotolewa siku a Alhamisi, 20 Februari 2014, Soma.
Picha na blog.bounzd.com
Kwa kuzingatia maombi ya wasomaji wetu, tumeonelea ni vyema tukamalizia njia nyingine 3 zilizobaki za kupambana na kumshinda mshindani katika biashara,  ikiwa wengi wamejaribu kuzitumia njia mbili zilizotolewa katika makala iliyopita kwa mafanikio ya kuboresha ushindani wa biashara zao.
Nasi bila hiyana leo tunamalizia njia hizo kama ifuatavyo;
 3.Ongeza thamani ya ubora 
Wafanyabishara wengi hufikiri kuwa wakishusha bei zaidi ya mpinzani watalishinda soko, 
La hasha! Ikiwa mfanyabiashara kafikia hatua hii ujue kasahau kuwa, wateja hununua thamani ya kitu kwa lugha ya Kiingereza “value” ikiwa na maana ya kumridhisha mteja na si gharama ya kitu.Chukulia mfano wa bidhaa na huduma za Kampuni ya Apple zilivyo na thamani ya ubora  inayoendana na gharama.
Ingekuwa wateja wanaangalia gharama, hakika watu wachache sana wangeweza kumudu.Ila kwa kuzingatia thamani ya ubora, watu wanajitahidi kumiliki bidhaa na huduma za Kampuni ya Apple.
Hivyo,ongeza thamani ya ubora ikiwa sanjari na ongezeko la bei zaidi ya mpinzani wako…Hakika utalishinda soko!

4.Thamini kila mteja
Usijaribu hata siku moja kumbeza mteja wa aina yeyote ile, huwezi kujua leo kanunua kitu cha sh.1000 kesho atanunua kitu cha sh.10,000 nakuendela.Pia ujue kuwa wateja wako wanachukua sehemu kubwa ya matangazo, tena wanakufanyia matangazo bure! kwa njia ya mdomo…ni kwa sababu umewauzia thamani ya ubora wa huduma na bidhaa. 
Hii ni njia nzuri ya kucheza na saikolojia ya wateja wako, wakati huo huo ukiendelea kumshinda mpinzani wako katika soko.

5.Weka motisha kwa mteja
Njia hii ni nzuri ikiwa unaifuata njia namba 4.Njia hizi mbili zinaendana sana.Bila kujali aina ya mteja, hakikisha unajua kwanza motisha zitolewazo na mpinzani/wapinzani wako.
Mifano tunayo mingi, hebu jaribu kuchunguza makampuni ya simu jinsi yanavyocheza na akili za wateja kwa kuweka vijimotisha kila kukicha.Lengo lao kubwa ni kuhakikisha unabaki kwenye kampuni ya simu husika.Hata kama makampuni yote yanatoa motisha, usihofu!…mteja ndiye mwenye chaguo, atahakikisha anapata motisha kutoka kila kampuni kulingana na huduma itolewayo kwa wakati husika.Nawe hutakuwa na kitu cha kupoteza.

Mwisho, ndugu msomaji na mfanyabiashara nikutakie kila la heri katika kuboresha na kuimarisha biashara yako, usije kulogwa kumchukia mpinzani wako, huyu anakusaidia sana kuboresha biashara yako na kuifanya isibaki kama ilivyo kwa miaka nenda rudi.Hivyo mjue undani wake, Soma na boresha thamani ya ubora.
Kwa ushauri na maelekezo ya biashara, usisite kuwasiliana nasi,
+255 754 572 143

Imetayarishwa na kutolewa na 
Jielimishe Kwanza!

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni