inspire

inspire

Lebo

AFYA (8) AJIRA (5) BIASHARA (39) ELIMU (14) MAHUSIANO (2) MALEZI (16) MAZINGIRA (12) SAIKOLOJIA (48) VIJANA (7)

Business registration

Green Consulting

business consultancy

business consultancy

Business consulting-2

Business consulting-2

Professional Consulting

PDC

Swahili translator

Swahili translator

TANGAZO-KITABU

E-BOOK: MTAZAMO WAKO NI UPI?

TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- .... TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- ....

TANGAZO TUWEZESHANE

TANGAZO TUWEZESHANE

DARDY'S INVST-20/10/2017

DUNIA IKUONE

DUNIA IKUONE

Jumanne, 4 Machi 2014

KAZI NA AJIRA: KUFANYA KAZI KWA BIDII PEKEE HAITOSHI…FANYA KWA MOYO!




“And the only way to do great work is to love what you do”-Steve Job
Njia pekee ya kufanya kazi kwa ufanisi ni kupenda kile unachofanya-Steve Job



 
Utendaji kazi na wenye tija ya mafanikio huanzia ndani ya moyo.Mtu anaweza kufanya kazi kwa bidii ila ndani ya moyo wake anasononeka na kuwaeleza wengine kuwa anapata ujira usiokidhi mahitaji yake.Hapa tunasema mtu huyu hana moyo wa kazi…
Picha:www.telegraph.co.uk
Watu wengi hufanya kazi wasizozipenda ilimradi tu wapate kipato kwa wakati husika, pia kwa sababu wamekosa kazi.Naomba nikuhakikishie ndugu msomaji, hakuna kitu kibaya kama kufanya kazi usiyoipenda! Ukifanya kazi usiyoipenda, hata kama unafanya kwa bidii vipi utajiona ni mtumwa tu.
Nikimnukuu Mama Theresa anasema; usitarajie mambo makubwa, tenda mambo madogo kwa moyo- kwa lugha ya kiingereza: “Don't look for big things, just do small things with great love.”Ukitenda mambo madogo kwa moyo ni rahisi sana kukupeleka kwenye mambo makubwa.Anasisitiza tena kuwa; Kufanya kazi pasipo upendo ni utumwa. “Work without love is slavery.”
Hapa nitatengeneza swali, moyo upi tena ikiwa natafuta kipato cha kukidhi mahitaji? Naweza kuliweka hili sawa kuwa, hupaswi kufanya kazi fulani usiyoipenda kwa minajili kuwa  ina kipato kikubwa…kama nilivyosema awali, utakuwa mtumwa wa kipato! Ndiyo maana kila siku wafanyakazi wanalalamika kuwa kipato hakitoshi, hii ni kwasababu wamejikita sana kwenye kuangalia maslahi pekee bila kuonyesha moyo wa kazi, pia hawalinganishi na ubora wa kazi wauletao kwenye soko.Kama alivyosema Jim Rohn kuwa, “watu hulipwa kutokana na uthamani wauletao kwenye soko.”Thamani kubwa zaidi kwenye soko, ujira mkubwa zaidi.Je, utawezaje kuleta uthamani kwenye soko kama huipendi kazi yako?
Ubora wa kazi hauwezi kupatikana kama watu wakitoa udenda kwanza kwenye kipato kabla ya kuonyesha moyo wa kujitoa na kuipenda kazi.Kwa lugha rahisi kabisa, onyesha moyo na nia ya kazi uifanyayo bila kutoa macho makubwa kwenye ujira.
Nimeshuhudia baadhi ya wafanyakazi wanaofanya kwa moyo- mh! Kama ukiwaona ndugu msomaji, unaweza kufikiri wanalipwa ujira mkubwa sana, lakini nilipopata fursa ya kuwahoji, wakanieleza kuwa wanafanya hivyo kwa sababu wanaipenda kazi, yaani wanajiona huru kufanya kazi.
Unaweza usinielewe kwa haraka haraka, fanya jaribio la kuipenda kazi kwanza, onyesha ubora, usinung’unike kama wengi wafanyavyo…utastaajabu kuona kipato kikiongezeka kwa njia nyingine.Utakuwa huru sana kwa sababu unajua sababu ya kufanya hivyo.
Ikiwa hujajua kazi uipendayo; jitathimini, isikilize sauti ya ndani ya moyo wako, chukua hatua ya kubadilika…simaanishi uache kazi, ila tenga muda wa ziada kuifanya kazi unayoipenda.
Kuna wakati mwingine nitakufahamisha faida za kufanya kazi unayoipenda.
Imetolewa na
Jielimishe Kwanza!
Kama unataka ushauri usisite kuwasiliana nasi, 
Barua pepe: jielimishekwanza@gmail.com 
Skype: JielimisheKwanza13
Facebook: Jielimishe Kwanza!
+255 754 572 143



Hakuna maoni:

Chapisha Maoni