inspire

inspire

Lebo

AFYA (8) AJIRA (5) BIASHARA (39) ELIMU (14) MAHUSIANO (2) MALEZI (16) MAZINGIRA (12) SAIKOLOJIA (48) VIJANA (7)

Business registration

Green Consulting

business consultancy

business consultancy

Business consulting-2

Business consulting-2

Professional Consulting

PDC

Swahili translator

Swahili translator

TANGAZO-KITABU

E-BOOK: MTAZAMO WAKO NI UPI?

TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- .... TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- ....

TANGAZO TUWEZESHANE

TANGAZO TUWEZESHANE

DARDY'S INVST-20/10/2017

DUNIA IKUONE

DUNIA IKUONE

Jumamosi, 15 Novemba 2014

MTAZAMO:

 USIDHARAU MAMBO YANAYOONEKANA KUWA NI MADOGO…


Ni mara nyingi jamii imekuwa ikipotezea sana masula au mambo yanayoonekana kuwa ni madogo "small things" kwa wakati husika.Inafika wakati natafakari, nashawishika, pia kuchelea kukumbuka na kuikumbusha jamii misemo hii ya Kiswahili inayoonekana kupitwa na wakati kama;  “mdharau mwiba mguu huota tende” na ule wa “usipoziba ufa utajenga ukuta”.
Katika kuendana na wakati, pia uhalisia wa mambo yatokeayo kila siku; misemo hiyo tajwa ina maana kubwa na kwa hakika haijapitwa, wala haitapitwa na wakati abadani.Misemo hiyo au “methali” za Kiswahili zilikuwepo na kutumika kuweka taadhali kwa mambo yanayoonekana kupuuzwa na kuwa ni mzaha ilihali mwisho wa siku madhara yake ni makubwa sana kuliko ilivyodhaniwa awali.
Nchini Tanzania na bila shaka kungineko duniani kuna tabia na mazoea yaliyojijenga ndani ya jamii yenye kupuuza masuala au mambo yanayoonekana kuwa madogo kwa wakati husika.Kuainisha baadhi ya masuala hayo ni kama;
·      kutupa takataka ovyo kwa minajili eti ni kidogo tu ikitupwa nje ukiwa ndani ya chombo cha usafiri haitakuwa na madhara yoyote
·      pia utupaji wa taka ngumu kiholela katika mazingira yetu
·      kuchoma na kukata miti ovyo bila urejeshaji wake
·      kutiririsha maji taka ovyo kwenye bahari na vyanzo vingine vya maji,
·  kutupa taka hewa angani kwa minajili kuwa zitasafiri kwa upepo na kwenda sehemu nyingine zikipungua madhara yake.Taka  hewa hizo ni kama hewa ukaa (CO2), na gesi taka nyinginezo za viwandani na vyombo vya usafiri vitumiavyo mafuta.
Nimeainisha masuala machache yanayochukuliwa kama mzaha na madogo sana kwa wakati uliopo, ila madhara yake ni makubwa kadiri siku zinavyoyoyoma.Madhara ya mambo yanayoonekana kuwa ni madogo hujikusanya kidogo kidogo bila jamii kutambua kwa wakati husika. Chukulia mfano halisi wa tatizo la mmong’onyoko wa udongo unavyotokea; huanza taratibu kwa udogo kuondolewa katika uso wa ardhi- katika eneo moja lililo wazi kwa kukosa miti na nyasi hadi eneo lingine kidogo kidogo kwa upepo na mvua, hatimaye kupelekea kuwepo kwa mabonde na ardhi isiyofaa kwa shughuli mbali mbali.
Pia kuna madhara mengine huripuka na kuiacha jamii na wataalamu kuhaha huku na huko kutafuta tiba ya matatizo yaliyosababishwa na mkusanyiko wa mambo madogo madogo. Mfano mwingine ni huu wa “wimbo wa dunia” wa “mabadiliko ya tabia ya nchi” yapelekeayo kuongezeka kwa joto duniani-kwa lugha ya huko majuu hujulikana kama “climate change” ni matokeo ya shughuli za kila siku za binadamu zenye kupuuza masuala madogo madogo kwa miaka nenda rudi.
Katika kipindi hicho cha kuhaha, msemo mwingine ndani ya jamii wa “kinga ni bora kuliko tiba” hujitokeza kama sehemu ya kujikumbusha uzembe uliotokea awali wa kudharau masuala na mambo yaliyoonekana kuwa ni madogo. Hapa jamii hukumbuka kujikinga na madhara yaliyotokea kwa kudharau mambo madogo.Kampeni nyingi zenye pesa hujitokea ili kuhamasisha mbinu mbadala za kujikinga na madhara yaliyotokana na mambo madogo, pia kujipatia matumaini ya kurejesha hali pendwa ilikuwepo awali.
Kiuhalisia, ni rahisi sana kufanikiwa kupambana na kupata suluhisho la mambo yapelekeayo madhara makubwa katika hali ya awali kabisa-hali ya udogo wake na si kupuuza udogo wake.
Hivyo basi, ni vyema na ni wajibu wa kila mwanajamii kutopuuza hata kidogo mambo au masuala yanayoonekana madogo kwa kujiridhisha upeo wetu kwa wakati husika.
Soma zaidi kujua ni nani anawajibu wa kutunza mazingira kwa kutopuuza mambo madogo madogo yaliyoanishwa.
Imetolewa na Jielimishe Kwanza! Social Enterprise kwa udhamini wa “Ide@Spot” na “Enviro-Forum”

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni