inspire

inspire

Lebo

AFYA (8) AJIRA (5) BIASHARA (39) ELIMU (14) MAHUSIANO (2) MALEZI (16) MAZINGIRA (12) SAIKOLOJIA (48) VIJANA (7)

Business registration

Green Consulting

business consultancy

business consultancy

Business consulting-2

Business consulting-2

Professional Consulting

PDC

Swahili translator

Swahili translator

TANGAZO-KITABU

E-BOOK: MTAZAMO WAKO NI UPI?

TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- .... TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- ....

TANGAZO TUWEZESHANE

TANGAZO TUWEZESHANE

DARDY'S INVST-20/10/2017

DUNIA IKUONE

DUNIA IKUONE

Jumanne, 25 Novemba 2014

MTAZAMO:


 USITEGEMEE KULIPWA SAWA SAWA NA WEMA ULIOTENDA…

Picha na http://www.simplemindfulness.com/2013/09/29/the-art-of-helping-others/
Watu wengi wamekuwa na mtazamo unaokinzana na ule usemi maarufu wa Kiswahili usemao; “tenda wema uende zako, usingoje shukrani”. Kupitia utafiti wa kimtazamo uliofanywa na Jielimishe Kwanza! Blog kuhusu kutenda mema kwa marafiki au ndugu umebaini kuwa 99.99% ya wanajamii nchini Tanzania hutarajia kurudishiwa wema ule ule waliomtendea mtu mwingine wakati wa shida au raha. Mfano mdogo tu ni wakati wa kutoa mchango wa harusi, watu hutoa mchango wakitarajia kuwa utamchangia vile vile kama alivyokuchangia.
Ifahamike kuwa, unapomsaidia ndugu au rafiki katika shida au raha ni sehemu mojawapo ya wewe kuonyesha ushirikiano na upendo kwa wanajamii kufanikiwa katika maswala mbali mbali.Isiwe kinyume chake kwa kumsaidia mtu na mwisho kutarajia malipo na yasipopatikana kama ulivyotarajia ni matusi na masimango-“eti fulani bwana nilimchangia na kufanikisha shughuli yake…yeye hakunichangia, watu wengine bwana! hawana shukrani!”
Pia inapaswa wanajamii kufahamu kuwa si kila anayekutendea wema umeweza kumlipa vile vile kama ulivyotendewa.Tunasaidiwa au watoto na ndugu zetu wa karibu wanasaidiwa na wengine kwa njia moja hadi nyingine kiasi kwamba tumeshindwa kurudishia wema ule ule.Ikiwa hali halisi ni hiyo, kwa nini sisi tuwe wa kwanza kudai shukrani kutoka kwa wenzetu?
Kiuhalisia ni kwamba tupo duniani ili tufaidiane, hakuna aliye mkamilifu wa kila kitu…hata hao wanasiasa na vigogo hutegemea sana wananchi wawaweke madarakani kwa kutoa ahadi kadha wa kadha, mwisho wa siku huwaacha solemba na kuwadharau kabisa hadi kipindi kingine cha kuomba na kubembeleza uongozi kifike.Sipigii makofi tabia hii hata kidogo! Namaanisha kuwa tuishi na watu vizuri tukijua maana na lengo halisi la kutegemeana na kufaidiana.Isiwe faida ya upande mmoja kila wakati, inapobidi toa shukrani kuthamini mchango wa wengine.Pia tunapotoa msaada au kutenda wema tusidai shukrani, kwa kuwa shukrani ya mtu iliyo ya dhati hugusa dhamiri ya mtu kwa kuzingatia uwezo wa wakati husika.
Nitofautiane pia na mtazamo wa wengine kuwa watendapo wema kwa mtu au watu ni kama wamewekeza; wakitarajia malipo ya shukrani vile vile kwa wema waliowatendea wengine.Ijulikane kuwa tutendapo wema kwa wengine tunajifungulia milango ya baraka kwa njia nyingine…bila kutarajia tunaweza kupata wema zaidi na usiopimika kupitia mlango mwingine kuliko kung’angana na kudai au kutegemea shukrani kutoka kwa wengine.
Hivyo basi, tusikate tamaa ya kuwasaidia wengine kwa kutotarajia malipo kutoka kwao.Tujitoe kwa raha na shida za wengine, wengine kupitia mlango usiofahamika watajitoa kutusaidia tukiwa na raha au shida.
Pia tunaposaidiwa, tuthamini sana mchango wa wengine kwetu; tukijitahidi sana kuwasaidia wengine kwa upendo tu ulio na ushirikiano wa dhati kwa wanajamii wengine na si kwa lengo la kulipiza wema ule ule kwa matarajio ya shukrani.
Imetolewa kwa udhamini wa Jielimishe Kwanza! Social Enterprise.





Hakuna maoni:

Chapisha Maoni