inspire

inspire

Lebo

AFYA (8) AJIRA (5) BIASHARA (39) ELIMU (14) MAHUSIANO (2) MALEZI (16) MAZINGIRA (12) SAIKOLOJIA (48) VIJANA (7)

Business registration

Green Consulting

business consultancy

business consultancy

Business consulting-2

Business consulting-2

Professional Consulting

PDC

Swahili translator

Swahili translator

TANGAZO-KITABU

E-BOOK: MTAZAMO WAKO NI UPI?

TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- .... TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- ....

TANGAZO TUWEZESHANE

TANGAZO TUWEZESHANE

DARDY'S INVST-20/10/2017

DUNIA IKUONE

DUNIA IKUONE

Jumanne, 16 Desemba 2014

MUENDELEZO:FANYA HIVI KUEPUKANA NA UTUMWA WA KISASA KATIKA MAENEO RASMI YA KAZI…



1.Boresha ujuzi wako wa kazi kwa kujiendeleza kwa siri ukilenga kuwa mfanyakazi makini mwenye mbinu stahiki za kazi. Kwa hatua hii utajiongezea uthamani sana katika eneo lako la kazi. Itafika wakati utamfanya mwajiri akuone ni wa thamani hivyo atajitajihidi asikupoteze. Ikifika hatua hii: Unaweza kujipangia aina ya mshahara kulingana na ubora ndani ya ajira husika.
2.Usionyeshe udhaifu wako kwa mwajiri. Usionyeshe kuwa unabembeleza sana ajira yake, ukifanya hivyo ni rahisi sana kutumikishwa kama mtumwa kwa sababu umeonyesha una dhiki.
3.Onyesha uwezo au kipaji chako kwa kadri uwezavyo. Kama unakumbuka, moja ya athari za utumwa wa kisasa ni kushindwa kuonyesha kipaji chako…hakuna mazingira rafiki ya utendaji kazi! Tumia kila mbinu kuhakikisha kipaji chako na uwezo wako wa kipekee unaonekana katika mazingira ya kazi. Ukifanikiwa, unganisha na mbinu namba 1 kujiongezea ubora zaidi katika kazi.
4.Acha kunung’unika chini chini! tenda, onyesha hisia zako kwa vitendo ukihitaji kuona mazingira rafiki ya kazi.Mweleze mwajiri wako kuwa hujapendezwa na mazingira yanayoendelea katika kazi.Wafanyakazi wengi wamekuwa ni waoga kuwaeleza waajiri wao yao ya moyoni kuhusu ujira waupato ukilinganisha na utendaji…wengi hawaridhiki na vipato vyao, wananung’unika chini kwa chini.Ondoa hofu! Ni wajibu na haki yako kujadiliana na mwajiri kuhusu ujira ili kuboresha utendaji kazi.
5.Ungana na kikundi cha wapinga “utumwa wa kisasa” katika maeneo ya kazi. Sauti ya wengi ina nguvu kubwa ya kuleta mabadiliko.
6.Tambua wajibu wako kwa kuhitaji “mpango wa kazi na majukumu kimaandishi” kutoka kwa mwajiri. Hakikisha unajiridhisha mapema kabla ya kuanza kazi. Majukumu uliyopewa yaendane na ujuzi ulio nao, pia yazingatie kipato unachopata.
7.Jielimishe zaidi kuhusu ajira na kanuni zake, haki za wafanyakazi kupitia vyombo mbali mbali vya habari.
8.Usifanye kazi kwa mazoea. Jitahidi kuwa mtu wa mabadiliko ukijiongezea uthamani katika soko la ajira.
Tukutakie kila la heri katika kujikomboa na utumwa wa kisasa katika maeneo rasmi ya kazi.
Imetolewa na 
Jielimishe Kwanza!

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni