inspire

inspire

Lebo

AFYA (8) AJIRA (5) BIASHARA (39) ELIMU (14) MAHUSIANO (2) MALEZI (16) MAZINGIRA (12) SAIKOLOJIA (48) VIJANA (7)

Business registration

Green Consulting

business consultancy

business consultancy

Business consulting-2

Business consulting-2

Professional Consulting

PDC

Swahili translator

Swahili translator

TANGAZO-KITABU

E-BOOK: MTAZAMO WAKO NI UPI?

TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- .... TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- ....

TANGAZO TUWEZESHANE

TANGAZO TUWEZESHANE

DARDY'S INVST-20/10/2017

DUNIA IKUONE

DUNIA IKUONE

Jumanne, 10 Februari 2015

MTAZAMO: FANYA HIVI KUKOSOA WENGINE BILA KULETA UGOMVI…


“I like oppositions and criticism, the two make me behave better with perfection-Henry Kazula
____________________________________________________________
Picha:managing-employee-performance.com
Napenda kukukumbusha ndugu masomaji wa Blog hii kuhusu moja ya makala zetu iliyobeba kichwa Ujasiriamali: wanaokupinga, kukudharau, kukuwekea vikwazo na kukukejeli wanakujenga bila wewe na wao kujijua…kwa mantiki kuwa hatupaswi kuogopa kukoselewa kwa minajili kuwa tutakatishwa tamaa au kudharaulika kwa maamuzi, mawazo au ubunifu wetu.

Katika safu hii leo napenda tuangazie upande mwingine wa yule au wewe unayependa kukosoa wengine kwa namna isiyo na lengo la kuboresha ubora wa utendaji ila kuwakwaza na kuwakatisha tamaa wengine. Yawezekana unafanya ukosoaji huo kwa kujua unachofanya au kwa kutojua uzito wa maneno yako kwa mhusika. 
Kwa kuzingatia mtazamo wa kisaikolojia, Jielimishe Kwanza! Blog inakudadavulia kinaga ubaga njia za kipekee za kukosoa wengine bila ya kumkwaza mhusika, wakati huo huo uhusiano ukiimarika na mhusika kujihisi vizuri na kutafakari kwa kina maoni aliyopewa.
Tumefanikiwa kukuletea njia 5 za msingi kuzitumia ili kuwa na uwezo wa  kukosoa kwa tija (constructive criticism) bila kuwakwaza wengine na sisi kujiongezea heshima na uthamani katika maeneo ya kazi;
1.    ANZA KWA KUTUMIA LUGHA ILIYO CHANYA…
DaleCarnegie, mwandishi wa kitabu “How to win Friends & Influence People” anasisitiza mtazamo chanya hasa katika kukosoa wengine bila kuleta ugomvi ukizingatia kuwa watu wengi hawapendi kukosolewa na hujiona wakamilifu muda wote.
Chukulia mfano wa kimtazamo ufuatao: Ikiwa umegundua kosa la kiutendaji au ni mapungufu tu ya kiutendaji kutoka kwa mfanyakazi unaweza kumwambia; “ukiongeza jitihada kidogo katika utendaji kazi wako utakuwa bora zaidi na kuongeza sifa ya kampuni” …na si kumwambia; sifurahishwi kabisa na utendaji kazi wako, ukiendelea hivyo nitakufukuza kazi”....
Au, unaweza kuwakuta watu wakitupa taka taka katika eneo lisilo rasmi ilihali kuna bango linaloonyesha sehemu sahihi ya kuhifadhi taka taka na kuwaambia; tafadhali naona ni vyema kama mngehifadhi taka taka zenu katika chombo kilichoonyeshwa…badala ya kusema; ninyi vipi! hamuoni bango linaloonyesha sehemu sahihi ya kutupa uchafu wenu? 
 
2.    ZINGATIA LENGO KUU KWA KUJENGA HOJA
Ni vyema kufahamu na kuzingatia sababu kuu ya wewe kukosoa mawazo au utendaji kazi wa wengine.Kwa kuzingatia lengo kuu utaweza kujua kwa kina maeneo yenye uzito na uhitaji wa maboresho zaidi, hivyo kutoa maoni yako yenye kukosoa kwa lugha iliyo rafiki.
3.    FUATILIA KWA UKARIBU UTEKELEZAJI WA MAONI YAKO
Si jambo baya ukimuona mhusika moja kwa moja na kumueleza ushauri wako juu ya utendaji kazi au mawazo fulani.Pia ukimuuliza mara kwa mara juu ya utendeaji kazi au utekelezaji wa maoni yako.Mhusika atakuona una lengo zuri la kutaka afanikiwe katika utendaji kazi.
4.    TAFUTA MUDA MUAFAKA WA KUKOSOA/KUTOA MAONI YAKO
Inapendeza kutafuta muda na mahali sahihi kumueleza mtu kuhusu mapungufu yake ya kiutendaji au mawazo ya kibiashara na si kuropoka mbele za watu kuhusu mapungufu yake. Inakera sana na kukatisha tamaa mara tu mtu anapokukosoa mahali pasipo sahihi au muda usio sahihi, haijalishi ubora wa ushauri kutoka upande mwingine.

5.    SIMAMIA UKWELI, USIFANYE KISHABIKI!
Tunapotoa ukosoaji haimaanishi kufanya ushabiki ili upande unaokosolewa ushindwe kutimiza malengo yake na kukata tamaa, la hasha! Lengo kuu ni kuhakikisha kuwa kunatokea maboresho chanya ya kiutendaji kutokana na ushauri au maoni yaliyotolewa.Ni vyema kuzingatia ukweli wa kila hoja ukizingatia lengo kuu la kuhamasisha utendaji na si kudhoofisha mawazo au utendaji kazi wa wengine.
Kuhusu kufanikiwa kuishi na watu vizuri na kuwahamasisha, Soma kitabu:
"How to Win Friends and Influence People" by Dale Carnegie.
Imetayarishwa na
Mwandishi wa Kitabu-Mtazamo Wako Ni Upi?
Imetolewa na
Jielimishe Kwanza.





Hakuna maoni:

Chapisha Maoni