inspire

inspire

Lebo

AFYA (8) AJIRA (5) BIASHARA (39) ELIMU (14) MAHUSIANO (2) MALEZI (16) MAZINGIRA (12) SAIKOLOJIA (48) VIJANA (7)

Business registration

Green Consulting

business consultancy

business consultancy

Business consulting-2

Business consulting-2

Professional Consulting

PDC

Swahili translator

Swahili translator

TANGAZO-KITABU

E-BOOK: MTAZAMO WAKO NI UPI?

TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- .... TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- ....

TANGAZO TUWEZESHANE

TANGAZO TUWEZESHANE

DARDY'S INVST-20/10/2017

DUNIA IKUONE

DUNIA IKUONE

Jumamosi, 14 Machi 2015

MTAZAMO: KABLA HUJAHUKUMU WENGINE JITATHIMINI KWANZA!

-->
Maisha yetu ya kila siku tunakumbana na maswahibu mbali mbali yanayopelekea fikra na utashi wetu kuchukua maamuzi rahisi na wakati mwingine maamuzi magumu sambamba na kutoa hukumu kwa yatokanayo.
Ukweli mchungu na usio na kificho ni kuwa, kila siku katika hali yetu ya kibinadamu tunakalia kiti cha heshima cha uhakimu na kutoa hukumu kuwahukumu wengine isivyo haki na kweli  kutokana na makosa yatokanayo na maamuzi yao; maamuzi rahisi au magumu.
Kuna jambo la msingi la kuzingatia kwanza ikiwa tupo kwenye kiti cha kutoa hukumu; ni la kiimani, Sawa! (kama inayovyoaminiwa na baadhi ya dini) kuwa usihukumu wengine kabla hujahukumiwa-Mungu pekee ndiye wa kuhukumu kwa haki pia kabla ya kuwahukumu wengine tujichunguze/tujitathmini wenyewe kwanza; je tu wasafi?, je tupo katika upande wa kutenda haki au upande wa kupenda kutendewa haki?

Pia, tunapoonyeshea wengine kidole kwa kuhukumu, itambulike kuwa kuna vidole vitatu vinatonyeshea sisi; hii ina maana kubwa sana katika uumbaji wa Mungu-tujitathmini sisi kwa kina kwanza kabla ya kutoa hukumu kwa wengine.
Sehemu hii imekuwa ya msingi sana ili tuweze kutoa hukumu za kibinadamu zilizo za haki na zisizo na mawaa, ilhali Mungu pekee ndiye anayehukumu kwa Haki na Kweli!
Binadamu kwa asili, tunahukumu masuala mbali mbali ili kukosoa na kujiridhisha nafsi zetu.Hukumu zetu huambatana na mtazamo hasi kuhusu wengine, mfano: naweza kuona ndugu au rafiki yangu amekata mawasiliano na mimi kwa muda mrefu, hii inasumbua akili yangu na mwisho nashindwa kuchelea kutoa hukumu kwa maneno hasi (bila kujitathmini mimi kwanza kama sijamkwaza)- kuwa ndugu/rafiki yangu ameanza dharau siku hizi, anajisikia sana, ananionea wivu ameona nimemzidi kimaisha, yeye ameona kuwa mimi sifai na si wa hadhi yake, ameona atuendani kiuchumi na mengine mengi; haya ni baadhi tu ya majibu rahisi ya kupoza hisia ingawaje sijui kama natoa hukumu ya haki na kweli juu yake. Je,  ni kweli ipo hivyo? Vipi kama ana matatizo? Mara ngapi nimefuatilia kujua kuhusu ndugu/rafiki yangu? Ni mfano tu ndugu hakimu mwenzangu ambao umewahi kunitokea…nimejifunza na ninaendelea kubadilika kwa hili.Natumaini nawe utafanya juhudi kwa hili.
Sawa, tunaweza kuona ni jambo jema kwa kufurahisha nafsi zetu na kuwakosoa wengine kwa mapungufu yao lakini jambo la kuzingatia na la msingi, narudia tena kwa msisitizo; tujitathmini wenyewe kwanza ili hukumu zetu ziendane na matakwa ya Yule aliye Hakimu wa Kweli na Haki.
 “Kumpatia mtu silaha asiyohitaji na asiyoweza kuitumia ni sawa na kutompa kabisa, pia ni hatari; inaweza kumdhuru” –HenryKazula.
Maarifa kwa wanaohitaji maarifa, pia walioonyesha nia ya kuhitaji maarifa.Onyesha uhitaji wa maarifa,tutakuelimisha kutumia vizuri maarifa uliyopewa.
Imetayarishwa na
Mwandishi wa Kitabu-Mtazamo Wako Ni Upi?
Imetolewa na
Jielimishe Kwanza.



Hakuna maoni:

Chapisha Maoni