inspire

inspire

Lebo

AFYA (8) AJIRA (5) BIASHARA (39) ELIMU (14) MAHUSIANO (2) MALEZI (16) MAZINGIRA (12) SAIKOLOJIA (48) VIJANA (7)

Business registration

Green Consulting

business consultancy

business consultancy

Business consulting-2

Business consulting-2

Professional Consulting

PDC

Swahili translator

Swahili translator

TANGAZO-KITABU

E-BOOK: MTAZAMO WAKO NI UPI?

TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- .... TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- ....

TANGAZO TUWEZESHANE

TANGAZO TUWEZESHANE

DARDY'S INVST-20/10/2017

DUNIA IKUONE

DUNIA IKUONE

Jumatatu, 9 Machi 2015

MTAZAMO: CHUNGUZA CHANZO CHA MATATIZO!


Picha na lauraecpaul.wordpress.com

Tunaishi katika dunia iliyozungukwa na matatizo kadha wa kadha yaliyo ya asili na mengine ni chanzo cha mwanadamu mwenyewe kwa kudharau mambo yanayoonekana kuwa ni madogo.
Matatizo yaliyopo huchochea fikra za mwanadamu katika kuelekea kutoa suluhisho au kutatua matatizo; mwisho wa siku imekuwa ni sehemu ya maisha yetu ya kila siku kupambana na kukuna vichwa kutatua matatizo.
Mtazamo tofauti umejengeka na kuzoeleka kwa wanajamii katika kuelewa na kutatua matatizo, wengi hutizama matatizo pekee na kukurupuka kutoa majibu rahisi ya matatizo kwa hisia bila kuyafahamu matatizo yenyewe kwa kina na kujali chanzo cha matatizo hayo kwa kufanya uchunguzi au utafiti wa kina.Hii ni sahihi kurejea msemo huu wa Kiswahili-“usiangalie umeangukia wapi,angalia ulipojikwaa”.
Katika ulimwengu huu tunaoishi kuna matatizo kama nilivyosema awali; matatizo yana chanzo chake kama ilivyobainishwa na msemo wa kisayansi katika sheria ya mwanafalsafa Socratic- na sheria yake ya “law of causality”“The Law of Cause & Effect states that absolutely everything happens for a reason.” sheria hii ikiainisha wazi kuwa kila jambo hutokea kwa sababu maalum.
Tukitupia jicho upande mwingine wa kutoa au kutafuta suluhisho la matatizo duniani, mwana fisikia maarufu duniani- Albert Einstein  anatukumbusha kuwa; “We cannot solve our problems with the same thinking we used when we created them.” Akimaanisha kuwa matatizo hayapatiwi suluhisho kwa uelewa wetu ule ule uliotumika kuyatengeneza-hivyo tunahitaji kufikiri tofauti.
Einstein anasisitiza tena kwa kujiweka mwenyewe katika kuchunguza na kuelewa matatizo kuwa-“If I had an hour to solve a problem I'd spend 55 minutes thinking about the problem and 5 minutes thinking about solutions.”-Akimaanisha kuwa ni vizuri kutumia au kujipatia muda wa kutosha (wa dakika 55) kufikiri na kuelewa tatizo na hatimaye kutumia muda mchache (wa dakika 5) kutoa suluhisho ikiwa angepata saa moja kutatua tatizo fulani.
Nikutie ujasiri ndugu msomaji, hatupaswi kuwa watu wa kulalamika au kukata tamaa kutokana na matatizo yaliyopo na yanayoendelea kuwepo.Tunapaswa kutumia utashi au akili binafsi tuliyopewa na Muumba wetu kufikiri na kuyaelewa matatizo kwa kina-hasa chanzo chake kupitia tafiti na njia mbali mbali zilizotumika na wengine kwa kujielimisha kwanza hatimaye kupata suluhisho sahihi la matatizo yetu.
Imetayarishwa na
Mwandishi wa Kitabu-Mtazamo Wako Ni Upi?
Imetolewa na
Jielimishe Kwanza.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni