inspire

inspire

Lebo

AFYA (8) AJIRA (5) BIASHARA (39) ELIMU (14) MAHUSIANO (2) MALEZI (16) MAZINGIRA (12) SAIKOLOJIA (48) VIJANA (7)

Business registration

Green Consulting

business consultancy

business consultancy

Business consulting-2

Business consulting-2

Professional Consulting

PDC

Swahili translator

Swahili translator

TANGAZO-KITABU

E-BOOK: MTAZAMO WAKO NI UPI?

TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- .... TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- ....

TANGAZO TUWEZESHANE

TANGAZO TUWEZESHANE

DARDY'S INVST-20/10/2017

DUNIA IKUONE

DUNIA IKUONE

Ijumaa, 19 Julai 2013

ELIMU NA MALEZI: MJENGEE MTOTO WAKO TABIA YA KUSOMA VITABU...

-->
Picha na www.pbs.org
Mzazi/Mlezi unaonekana kama kioo kwa mtoto.Mtoto anajifunza mengi kupitia wewe, pia anaamini mafundisho yako. 
Tukizungumzia utamaduni wa kusoma vitabu vyenye tija ya kuelimisha, ni muhimu sana kumjenga mtoto wako akiwa katika umri unaoendana na hatua ya kutaka kujua mambo mengi- hasa kwa kukuuliza maswali mbali mbalimbali.Toa majibu mazuri kwa mtoto ukiambatanisha na maarifa kutoka kwenye vitabu.

Kwa sasa najua sio tatizo tena kwa mzazi kusoma kitabu chenye tija ya maendeleo, hasa ukizingatia somo lilitolewa kupia makala ihusuyo mbinu 10 za kuanza kusoma kitabu chenye tija ya maendeleo kupitia http://jielimishekwanza.blogspot.com/2013/07/elimu-na-mtazamo-mbinu-10-za-kuanza.html?utm_source=BP_recent
Leo naomba ufuate nami katika hatua nyingine ya ujasiri na yenye mafanikio katika kumjengea mtoto wako uwezo na shauku ya kuwa msomaji wa vitabu.

1.     Kuwa mfano wa kuigwa katika kusoma kitabu…weka utaratibu unaoleweka na kufuatwa na familia kuhusu usomaji (najua hili sio tatizo tena kwa kuwa umesoma na kuzifanyia kazi mbinu 10 kupitia http://jielimishekwanza.blogspot.com/2013/07/elimu-na-mtazamo-mbinu-10-za-kuanza.html?utm_source=BP_recent
2.     Msomee mtoto wako kitabu na kumsaidia sehemu zenye utata (Zingatia umri na uelewa wa mtoto)

Picha na home-startwigtownshire.co.uk

3.     Mwekee mtoto utaratibu wa kusoma kitabu na kuwasilisha taarifa fupi mara amalizapo sehemu ya kitabu au kitabu chote…soma zaidi http://jielimishekwanza.blogspot.com/2013/07/malezi-na-elimu-ukitaka-mtoto-wako.html (Zingatia umri na uelewa wa mtoto)
4.     Jenga utamaduni wa kununua vitabu mbali mbali vyenye kuchochea maarifa kwako na kwa mtoto( unaweza kuweka utaratibu wa kununua vitabu 3-5 kwa mwezi)

5.     Mpongeze mtoto anapoonyesha juhudi ya kusoma kitabu-chagua zawadi zinazochochea usomaji zaidi mfano kumpeleka sehemu tulivu ya kuvutia ili kujisomea na kuburudika.(Zingatia hali ya kipato chako-huna sababu ya kujitetea, zipo sehemu nzuri za mapumziko zisizohitaji hata pesa)

Hongera sana kwa kutimiza zoezi hili!

Maarifa mengi sana yamefichwa kwenye vitabu…
Yapekue! Yasome!Yaelewe!Yafanyie kazi kwa dhati hasa yale yanayofaa kwa wakati husika.

Imetolewa na
Jielimishe Kwanza!
Ikiwa una maoni au una hitaji ushauri kuhusu usomaji wa vitabu ulio na manufaa,usisite kuwasiliana nasi. Hakuna gharama ya huduma hii!
0785 175 157                             Barua pepe:jielimishekwanza@gmail.com