inspire

inspire

Lebo

AFYA (8) AJIRA (5) BIASHARA (39) ELIMU (14) MAHUSIANO (2) MALEZI (16) MAZINGIRA (12) SAIKOLOJIA (48) VIJANA (7)

Business registration

Green Consulting

business consultancy

business consultancy

Business consulting-2

Business consulting-2

Professional Consulting

PDC

Swahili translator

Swahili translator

TANGAZO-KITABU

E-BOOK: MTAZAMO WAKO NI UPI?

TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- .... TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- ....

TANGAZO TUWEZESHANE

TANGAZO TUWEZESHANE

DARDY'S INVST-20/10/2017

DUNIA IKUONE

DUNIA IKUONE

Jumatano, 28 Agosti 2013

MTAZAMO NA UCHUMI: JINSI YA KUWA NA MALI KWA KIPATO KIDOGO ULICHONACHO…

Picha  na endoftheamericandream.com
Hivi umewahi kujiuliza kwa nini matajiri wanaendelea kuwa matajiri wakati huo huo masikini wanaendelea kuwa masikini?
Tofauti kati ya makundi haya mawili ni kwamba, matajiri wanawekeza zaidi kwa kutumia pesa zao wakati huo huo masikini wanatumia ovyo kwa kile wanachokipata.
Nikilinganisha hali hii kihistoria, hasa maisha ya zamani ya babu na bibi zetu kutegemea uwindaji, ilikuwa ni hali iliyozoeleka kwa wanaume kuaga familia zao asubuhi na mapema kwenda kutafuta kitoweo.Hii ilikuwa ni hali ya kila siku ili kuweza kukidhi haja ya siku husika.
Kwa jamii za wale waliogundua siri ya kujilimbikizia mali waliamua kutengeneza boma la kuhifadhia wanyama waliowategemea kwa mlo…hapa ufugaji ukaanza, kwa lengo la kujiepusha na usumbufu wa kwenda kuwinda mara kwa mara pia uhaba wa wanyama kwa msimu fulani.Baada ya muda fulani wanyama waliowafuga walizaliana na hatimaye kukidhi hitaji la kitoweo pia kuuza kwa wengine wasiokuwa na maono ya kujilimbikizia kwa ajili ya baadaye.
Historia inatufundisha kujiwekea akiba ya baadaye na si kuangalia maisha ya leo.
Kuna hatua mbili (2) muhimu wanazotumia watu wenye mali nyingi na kuendelea kuwa jinsi walivyo:
1.KUWA NA MAAMUZI SAHIHI YA KUTUMIA PESA KATIKA NJIA SAHIHI... mfano kununua kitu kwa kusudi maalumu na si kwa sababu imetokea tu au kwa sababu mtu mwingine anacho au tu kwa mashindano..la hasha!
2.KUJENGA “BOMA”
Kama nilivyotoa mfano wa kihistoria kuhusu maisha ya watu wenye mali waliowahi kuishi, kwa maisha ya leo kuna mifumo mbali mbali ya kuwa na boma nayo ni;
·  KUJENGA BIASHARA
· KUTUNZA PESA (AU KUTUNZA VITU VINAVYOWEZA KUTHAMANISHWA NA PESA WAKATI PESA IKIHITAJIKA)
· KUJIHUSISHA NA KUNUNUA VIWANJA, NYUMBA NA KUKODIAHA/KUPANGISHA AU KUUZA KWA FAIDA
·    KUWEKEZA KWENYE SOKO LA HISA

Makala hii imeandaliwa na Jielimishe Kwanza! kwa kushirikiana na kitabu alichoandika mjasiriamali maarufu nchini Marekani Robert Kiyosaki-“Be Rich & Happy”  Sura ya 19 ukurasa wa 195.  

Ikiwa unahitaji kitabu hicho tuwasiliane kupitia 0754 572 143.Ikiwa unaona uvivu kusoma kitabu, fuatilia mbinu za kuanza kusoma kitabu kwa mafanikio kupitia http://jielimishekwanza.blogspot.com/2013/07/elimu-na-mtazamo-mbinu-10-za-kuanza.html
Usipuuze ushauri huu, kumbuka maneno ya tajiri mkubwa -Henry Ford, mwanzilishi wa kampuni ya magari aina ya Ford alisema; 

"PAYING ATTENTION TO SIMPLE LITTLE THINGS THAT MOST MEN NEGLECT MAKES A FEW MEN RICH " -Henry Ford