inspire

inspire

Lebo

AFYA (8) AJIRA (5) BIASHARA (39) ELIMU (14) MAHUSIANO (2) MALEZI (16) MAZINGIRA (12) SAIKOLOJIA (48) VIJANA (7)

Business registration

Green Consulting

business consultancy

business consultancy

Business consulting-2

Business consulting-2

Professional Consulting

PDC

Swahili translator

Swahili translator

TANGAZO-KITABU

E-BOOK: MTAZAMO WAKO NI UPI?

TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- .... TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- ....

TANGAZO TUWEZESHANE

TANGAZO TUWEZESHANE

DARDY'S INVST-20/10/2017

DUNIA IKUONE

DUNIA IKUONE

Jumanne, 15 Oktoba 2013

MTAZAMO: SIMU YAKO NI IPI KATI YA HIZI?


W
 abunifu wa simu za mkononi wamekuwa wajanja sana kwa kucheza na fikra na mtazamo wa watumiaji. Ukiangalia kwa makini lengo la simu hizo linabaki pale pale-KUWASILIANA! haijalishi ni simu ya aina gani-iwe ya gharama kubwa au ndogo.


Katika kipindi kifupi wabunifu hao wamefanikiwa kuteka fikra za watumiaji wengi duniani kwa kuongezea vikolombwezo mbali mbali vya matumizi kama vile “Internet”, mfumo wa kutumia ujumbe wa moja kwa moja kama Whatsup! Na mengineyo yanayowapendezesha watumiaji kama kioo cha kugusa (kubonyeza ni shida!) na muonekano mzima wa simu.
Maboresho hayo ya simu kulingana na mitindo ya yote niliyotaja hujumuisha ongezeko la gharama -( mfano kuna simu inayofikia hadi Shilingi milioni mbili za Kitanzania).
Kulingana na mvuto wa simu hizo, makundi yote ya watu kiuchumi yamekuwa yakivutika kwa kasi kununua simu hizo za gharama kubwa.Yaani kwa lugha nyingine watu wameamua kufanya uwekezaji katika simu zao za mkononi.Bila kujua, watu wamesahau lile lengo la msingi la simu za mkononi la KUWASILIANA!
Ni kawaida kabisa kumuona mtumiaji wa simu, akimiliki simu zaidi ya moja zenye gharama kubwa…wakati huo huo maisha yake yakiwa duni.
Taarifa za hivi karibuni kutoka nchini Denmark na nchi nyingine za Ulaya zimethibitisha kuwa watu wamekumbwa na msongo wa mawazo kutokana na simu zao za mkononi “smartphone” (hasa kutumia muda mrefu kuperuzi kupitia mitandao ya kijamii -facebook, twitter n.k) pia kutokana na wimbi kubwa la mabadiliko ya teknolojia sanjali na simu za mkononi “smartphone” wakati huo huo wakitakiwa kufanya kazi na kuwasiliana na watu wanaowapigia simu. Kwa sasa baadhi ya watumiaji wengine wa simu hizo wameanza kurudia tena kutumia simu zenye matumizi rahisi.
Pia soma hii http://jielimishekwanza.blogspot.com/2013/06/jamii-na-mawasiliano.html uone simu za mkononi zilipotufikisha.
Ushauri wa bure: 
Ni vyema kuchukua hatua ya kujiuliza maswali haya ya msingi kabla ya kuwa na wazo la kununua simu mpya; 
  • Nanunua simu hii ili na mimi nionekane ninazo ilihali sina pesa?
  •  Nawekeza kiasi gani cha pesa kwenye simu yangu? Je, simu hii itakuwa inarudisha faida au itakuwa rasilimali isiyozalisha na yenye kutoa pesa mfukoni mwangu mara kwa mara?
  •  Simu ninayonunua itanisaidia kwenye masuala ya kazi na biashara kwa kuongeza ufanisi na kipato?
Huu ndiyo uhalisia, ni mtazamo tu! Tuangalie sana, tunapaswa kuwekeza kwenye mipango endelevu ya maendeleo na si kwenye mitindo ya simu inayoingia kila kukicha. Lakini siyo mbaya kama unawekeza kwenye simu yako bila kusahau maendeleo endelevu ya kijamii. 

Soma hii http://www.medscape.com/viewarticle/804666 pia kujua zaidi kuhusu matumizi ya "Smartphone".
Imetolewa na 


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni