inspire

inspire

Lebo

AFYA (8) AJIRA (5) BIASHARA (39) ELIMU (14) MAHUSIANO (2) MALEZI (16) MAZINGIRA (12) SAIKOLOJIA (48) VIJANA (7)

Business registration

Green Consulting

business consultancy

business consultancy

Business consulting-2

Business consulting-2

Professional Consulting

PDC

Swahili translator

Swahili translator

TANGAZO-KITABU

E-BOOK: MTAZAMO WAKO NI UPI?

TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- .... TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- ....

TANGAZO TUWEZESHANE

TANGAZO TUWEZESHANE

DARDY'S INVST-20/10/2017

DUNIA IKUONE

DUNIA IKUONE

Alhamisi, 10 Oktoba 2013

VIJANA: KUJITOLEA - NJIA KUELEKEA KUPATA AJIRA NA UZOEFU WA KAZI


D
 hana ya KUJITOLEA inaonekana ni mpya sana kwa nchi mbali mbali za Kiafrika.Nikichulia mfano nchini Tanzania, vijana wengi wenye sifa za kupata ajira wanakaa nyumbani kusubiri wajibiwe maombi waliyotuma katika taasisi mbali mbali zinazotegemewa sana kwa kutoa ajira. Wakati huo huo wanasahau kuwa ujuzi wao unaendelea kupungua siku hadi siku. Pia kuna vijana wengine wasio na elimu ya kazi ila wana vipaji wapo vijiweni wakiendelea kufifisha vipaji vyao.

Jielimishe Kwanza! imefuatilia kwa kina dhana ya nzima ya KUJITOLEA na kuona kuwa kuna faida nyingi zinazoweza kupatikana kwa kijana kuchukua hatua ya uthubutu kuanza KUJITOLEA.Faida hizo ni; 

  1.      Kupata uzoefu wa kazi unayofanya…hivyo kigezo cha uzoefu kazini haikitakuwa kikwazo cha wewe kupata kazi
  2.       Utajifunza mbinu mpya za kazi
  3.       Kujiongezea wigo wa kufahamiana na watu katika kazi unayofanya
  4.      Ni njia mojawapo kukuunganisha na kazi nyingine
  5.      Utaifurahia kazi unayofanya kwa sababu unaipenda
  6.       Unajiongezea hali ya kuaminika kupata kazi

http://lindsayolson.com/5-reasons-you-should-volunteer-to-find-a-job/
Vijana wengi hujiuliza, naanzaje KUJITOLEA bila kulipwa chochote? Jibu ni rahisi kabisa, anza kujiangalia una ujuzi/kipaji gani? Pia angalia changamoto zilizopo kwenye jamii…FIKIRI kwa makini! Unaweza kufanya nini kulingana na ujuzi au uwezo wako kutatua changamoto zilizopo.

Narudia tena FIKIRI! tena kwa mapana(Uwe na taswira kubwa) ANZA kidogo kulingana na uwezo wako ukizingatia kiasi kidogo cha pesa ulicho nacho.Tambua kuwa, mabadiliko makubwa huanzia na jitihada ndogo ya mtu mmoja. 
Chukulia mfano wa mtu kama Mahtma Gandhi alivyoweza kuleta mabadiliko makubwa nchini India.Alituachia msemo huu maarufu duniani  Be the change that you wish to see most in your world”-Mahatma Gandhi.-Uwe chanzo cha mabadiliko utakayo kuyaona.

ANZA SASA! kwa  kujiweka, kujitokeza sehemu zenye fursa ili uonekane…TAMBUA kuwa FURSA HAIKUTAFUTI! JITOKEZE KUONA FURSA! Soma hii. http://jielimishekwanza.blogspot.com/2013/09/somo-kupitia-mimeatafuta-fursa-uonekane.html

Huna sababu ya kutembea na bahasha au kushinda ukipezi kutafuta nafasi za kazi mtandaoni au magazetini.Tambua kuwa kazi nyingi hutolewa kwa kufahamiana.

Najua mwanzo mgumu! Fahamu kuwa hakuna kitu kinapatikana kiurahisi…ukiona kipo cha urahisi kina shaka! Ni lazima utalipia gharama…Waingereza wanasema  hivi “you will pay the price nothing is for free”

Nikutie moyo zaidi kijana uliyekata tamaa ya kupata ajira kupitia nukuu maarufu ya mwandishi na msemaji wa hadhara- Zig Ziglar anasema(na si alisema, kwa sababu maneno yake yanaishi)  “You will get all you want in life if you help enough other people get what they want”- Zig Ziglar.(Utapata ukitakacho maishani kwa kuwasaidia wengine kikamilifu kupata wanachotaka).

Angalizo:
  • Usisahau kuwa Jielimishe Kwanza! inahitaji watu wa kujitolea "Volunteers" katika njanya ya Uandishi wa makala zenye mtazamo chanya na kuhamasisha utendaji bora wa kazi.
Tuwasiliane:          0716 075 826                                              jielimishekwanza@gmail.com

Imetayarishwa na kutolewa na






Hakuna maoni:

Chapisha Maoni