inspire

inspire

Lebo

AFYA (8) AJIRA (5) BIASHARA (39) ELIMU (14) MAHUSIANO (2) MALEZI (16) MAZINGIRA (12) SAIKOLOJIA (48) VIJANA (7)

Business registration

Green Consulting

business consultancy

business consultancy

Business consulting-2

Business consulting-2

Professional Consulting

PDC

Swahili translator

Swahili translator

TANGAZO-KITABU

E-BOOK: MTAZAMO WAKO NI UPI?

TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- .... TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- ....

TANGAZO TUWEZESHANE

TANGAZO TUWEZESHANE

DARDY'S INVST-20/10/2017

DUNIA IKUONE

DUNIA IKUONE

Jumatano, 6 Novemba 2013

MTAZAMO: KISAIKOLOJIA, KUMWAMBIA MTOTO/MWANAFUNZI KUWA WEWE NI SIFURI, NI SAWA NA KUUA KIPAJI CHAKE…

Picha na ii4oc.com

N
ikiutazama mfumo wa elimu hasa kwa nchi za Kusini mwa jangwa la Sahara, umelenga sana katika ufaulu wa masomo ya kitaaluma ili mwanafunzi aanze safari yake kujikomboa kimaisha bila kuangalia kipaji cha mwanafunzi husika, ikimaanisha kuwa taaluma kwanza, kipaji baadaye.

Imezoeleka kuwa ili mtu afanikiwe katika maisha yake ni lazima afaulu sana katika masomo yake awapo shuleni.Vipi kuhusu kutambua na kukuza kipaji cha mtoto/mwanafunzi bila kuangalia masomo ya kitaalamu? Ikiwa kuna ushahidi wa kutosha wa watu  maarufu waliotumia vipaji vyao kujiajiri pia kuajiri wengine, tunaweza kuliona hili kwa mtazamo mwingine chanya wa mabadiliko katika elimu.
Ukiangalia nchi nyingi zilizoendelea kiuchumi, hazijapuuza hata kidogo kipaji alichonacho mtoto/mwanafunzi…wanaangalia kwanza akipendacho mtoto kulingana na kipaji chake.Kuanzia hapo mtoto huanza kukuzwa kwa kujitambua na kunoa kipaji chake.
Masomo mengine ya utaalamu huchukuliwa kama ziada.Mtazamo huu ni mzuri kwa sababu mtoto/mwanafunzi akishindwa kufanikiwa katika masomo yake ya kawaida(masomo ya utaalamu), anajikita moja kwa moja katika kuonyesha kipaji chake kilichonolewa.
Nikitoa mfano halisi nchini Tanzania, wataalamu wa masula ya elimu wamekuwa na mtazamo kuwa ili mtoto afanikiwe maishani ni lazima apate matokeo kuanzia daraja la I hadi la III.Kuna kundi la wanafunzi wengine wa daraja IV na wale wa daraja 0…je vipi kuhusu hawa? Ni kweli hawawezi kufanikiwa maishani? Vipi kama kutakuwa na utaratibu wa kuchunguza na kutambua vipaji vyao ili vitumike kujiletea kipato? 
Katika siku za hivi karibuni, nchini Tanzania,Wizara ya elimu na mafunzo ya ufundi ilitoa tamko la kubadili madaraja na viwango vingine vya ufaulu.Lililokereketa umma wa wananchi na wataalamu wengine wa masula ya elimu ni lile la kubadili jina tu la divisheni 0 kuwa divisheni V.
Nikirejea mtazamo wa kisaikolojia, mtoto/mwanafunzi akiambiwa kuwa wewe ni “sifuri” inamjenga kuwa katika dunia hii yeye hawezi kufanya lolote akijilinganisha na wengine.
Mtazamo wa Jielimishe Kwanza! kuhusu badiliko la divisheni sifuri kuwa divisheni V ni kwamba,  badiliko la jina halitabadilisha alama la kundi hilo bali ni kumpoza mwanafunzi kisaikolojia ili asijione kuwa hawezi kabisa.Hivyo basi anaweza kufanya kitu kingine nje ya mfumo rasmi wa elimu uliomtenga kitaaluma na si kipaji chake.
Imefika wakati muafaka wa kuhamasisha wadau wote wa elimu kulitazama suala la kipaji cha mtoto/mwanafunzi kuwa kipaumbele kabla ya masomo ya kitaaluma, pia ni vyema kumfundisha mtoto/mwanafunzi kwa kile alichonacho, anachokifahamu, anachoweza kufanya kwanza. Hii itamsaidia mtoto/mwanafunzi kuwa na wigo mpana wa kufanya kile moyo wake unapenda kwa ufanisi mkubwa.
_______________________________
“Sometimes we fight who we are, struggling against ourselves and our natures. But we must learn to accept who we are and appreciate who we become. We must love ourselves for what and who we are, and believe in our talents.” Harley King
________________________________________________________________________________
Imetayarishwa na kutolewa na
Jielimishe Kwanza!










Hakuna maoni:

Chapisha Maoni