inspire

inspire

Lebo

AFYA (8) AJIRA (5) BIASHARA (39) ELIMU (14) MAHUSIANO (2) MALEZI (16) MAZINGIRA (12) SAIKOLOJIA (48) VIJANA (7)

Business registration

Green Consulting

business consultancy

business consultancy

Business consulting-2

Business consulting-2

Professional Consulting

PDC

Swahili translator

Swahili translator

TANGAZO-KITABU

E-BOOK: MTAZAMO WAKO NI UPI?

TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- .... TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- ....

TANGAZO TUWEZESHANE

TANGAZO TUWEZESHANE

DARDY'S INVST-20/10/2017

DUNIA IKUONE

DUNIA IKUONE

Jumatatu, 11 Novemba 2013

VIJANA NA VIPAJI: Mkurugenzi mtendaji wa Jielimishe Kwanza! azindua “Evening Talk Program”



I
likuwa ni wakati mzuri kwa Jielimishe Kwanza! kupata fursa ya kushirikiana na Taasisi nyingine katika masuala mbali mbali ya kijamii.
 Asasi isiyo ya kiserikali ijulikanayo kwa jina “Human Talent Watch" (H.T.W) iliyopo Mbezi-Msuguli- jijini Dar es salaam imeanzisha program maalumu ya kuibua na kukuza vipaji kwa vijana ijulikanayo kwa jina la “Evening Talk Program” ikimaanisha “maongezi rasmi ya jioni “ kwa kuwashirikisha watu waliofanikiwa kwa kutumia vipaji ili kuwatia moyo na kuwapatia mbinu  vijana chipukizi katika vipaji husika.

Programu hiyo maalumu na yenye tija kwa vijana wenye vipaji nchini Tanzania ilizinduliwa Jumamosi , 9 Novemba 2013 na Mkurugenzi mtendaji wa Jielimishe Kwanza! ndugu Henry Kazula majira ya jioni.

Akiongea moja kwa moja na mwandishi wa Jielimishe Kwanza! mwenyekiti wa H.T.W ndugu Frank Mihayo alifanunua zaidi malengo ya “Evening Talk Program”, alisema;

…programu hii ni maalumu kwa kuwakutanisha vijana wenye umri kuanzia miaka 12-35 pamoja ili kujifunza/kupata mbinu mbali mbali zitakazowasaidia kutimiza ndoto zao. ”Evening Talk” ni chimbuko la la maarifa sahihi kwa vijana-“a source of perfect knowledge”.Pia ni fursa maalumu kwa vijana chipukizi wenye vipaji kukutanishwa na vijana mashuhuri waliofikia mafanikio ya ndoto zao katika nyanja mbali mbali-sanaa,uchumi,uongozi na biashara.

Ndugu Mihayo alikazia zaidi kuwa, watu waliofanikiwa kwa vipaji vyao watapata fursa ya kutoa mada zenye kuchochea hamasa ya mafanikio kwa vijana kupitia vipaji. Kwa vijana chipukizi watapata fursa ya kujijengea hali ya kujitambua,kujiamini,kujifunza mambo mapya kuhusiana na vipaji na kupata nafasi kuunganishwa na wadau mbali mbali.

Katika kutimiza azma ya mpango huu kuna changamoto zifuatazo;

  1.       Kukosa ukumbi wa kuendeshea programu hii
  2.       Ukosefu wa fedha za uendeshaji kama kalamu na madaftari ya kuhifadhia kumbukumbu
  3.      Fedha ya kuitangaza programu hii kwenye vyombo vingine vya habari ili vijana wengi wapate fursa ya kushiriki na kujifunza.
 ____________________________


MATUKIO KATIKA PICHA

Mkurugenzi mtendaji wa Jielimishe Kwanza! ndugu Henry Kazula akikata utepe kuashira kuzinduliwa kwa programu maalum kwa vijana ijulikanayo kama "Evening Talk".Kulia kwake ni Mwenyekiti wa H.T.W ndugu Frank Mihayo.


Mkurugenzi mtendaji wa Jielimishe Kwanza! ndugu Henry Kazula akiongea na vijana wenye



vipaji vya mpira,muziki na uigizaji.




Katika nyuso za furaha vijana wenye vipaji vya muziki,uigizaji na mpira wakiwa na Mkurugenzi mtendaji wa Jielimishe Kwanza! ndugu Henry Kazula kwa pamoja na Mwenyekiti wa H.T.W ndugu Frank Mihayo.



Mwisho wa yote, mgeni rasmi alipewa fursa ya kuongea na vijana; alijaribu kuwashirikisha kwa kurejea moja ya makala zake kupitia Jielimishe Kwanza! ijulikanayo kwa kichwa

“Jinsi ya kupaza sauti ya mafanikio na jamii ikukubali" Soma hii  http://jielimishekwanza.blogspot.com/2013/05/jinsi-ya-kupaza-sauti-ya-mafanikio.html

Ikiwa umeguswa na program hii na unataka kuchangia kwa njia moja au nyingine usisitize kuwasiliana na Mwenyekiti wa H.T.W kwa namba +255 752 297 264 au muandikie kupitia barua pepe humantalentwatch@gmail.com

Imetayarishwa, Imetolewa na
Jielimishe Kwanza!






Hakuna maoni:

Chapisha Maoni