inspire

inspire

Lebo

AFYA (8) AJIRA (5) BIASHARA (39) ELIMU (14) MAHUSIANO (2) MALEZI (16) MAZINGIRA (12) SAIKOLOJIA (48) VIJANA (7)

Business registration

Green Consulting

business consultancy

business consultancy

Business consulting-2

Business consulting-2

Professional Consulting

PDC

Swahili translator

Swahili translator

TANGAZO-KITABU

E-BOOK: MTAZAMO WAKO NI UPI?

TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- .... TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- ....

TANGAZO TUWEZESHANE

TANGAZO TUWEZESHANE

DARDY'S INVST-20/10/2017

DUNIA IKUONE

DUNIA IKUONE

Jumapili, 2 Novemba 2014

MTAZAMO:NINI HASA HUKUAMINISHA KUWA HABARI KUTOKA CHOMBO FULANI CHA HABARI NI KWELI?

Ndugu msomaji natumaini u buheri wa afya na yawezekana unaendelea kufuatilia habari kem kem ili hali uwe jirani na dunia.Sambamba na hilo naomba nikukumbushe kidogo kuhusu makala yetu ya siku chache zilizopita kuhusu “je unajuaje kama kila unachoambiwa ni kweli?”  ukizingatia kuwa tunapenda kupata habari mpya kila siku.Tuliona kuwa ni vyema kuchunguza kwa kina na kujielimisha zaidi  kwa kusoma vitabu, makala, majarida mbali mbali na pia kusikiliza hotuba mbali mbali  ili kuboresha upeo wetu katika kupambanua mambo, mwisho wa siku kuweza kujua ukweli wa mambo.Kinyume na hapo tutakuwa ni watu wa kudanganywa tu, mwisho kuchukua maamuzi yasiyo sahihi kwa wakati husika!
Picha;http://www.tmf.or.tz/
Leo nataka nikulete kwenye mandhali hiyo hiyo lakini nikijikita zaidi katika taarifa lukuki tuonazo na kusikia kupitia vyombo mbali mbali vya habari vinavyojulikana na kuheshimika kisheria.
Ama kwa hakika tumekuwa mstari wa mbele kufuatilia kwa makini na kutaka kujua zaidi undani masuala mbali mbali yanayojili na yaliyojili ndani na nje ya nchi kupitia vyanzo hivyo vya habari.Inafika wakati tunabaki njia panda, hasa kwa kupata habari zilizo na mkakanganyiko na uzushi. Wakati mwingine tunagundua kuwa vyanzo vingine vya habari hutoa na kupambisha habari  ili viuze au kuboresha umaarufu wa watu fulani.
Wengi waweza kukubaiana nami kuwa kuna wakati habari tunazosoma kupitia magazeti na majarida…(sina haja ya kuyataja) huweka"headlines" / vichwa vya habari vya kuvutia sana lakini undani wa habari hukinzana kabisaaaa!!!! na hali halisi na matarajio ya msomaji.
Pia kwa upande wa televisheni zetu, ndugu msomaji unaweza kuwa shahidi; kuna mazingira ya habari na matukio yanayoonyeshwa wakati mwingine kwa maslahi ya watu fulani ili kujiimarisha kisiasa na kiuchumi na hata kutaka kuwa maarufu.Lakini ukizingatia na kufanya utafiti wa kutosha utaujua ukweli wa mambo kwa KUJIELIMISHA.
Ndugu msomaji, sina hakika sana kuwa ni mara ngapi umewahi kujiuliza swali hili ambalo leo nauliza; “nini hasa hukuhamasisha kuwa habari kutoka chombo fulani cha habari ukipendacho ni kweli?
Katika kutoa msaada wa kuweza kujibu swali hili ni vyema ukasoma tena makala yetu kuhusu “ je unajuaje kama kila unachoambiwa ni kweli?” utaona mbinu ya kuweza kuchuja habari tupokeazo kwa kusikiliza, kutazama na kusoma.Ila, mbinu kubwa kuliko zote ni ile ya kufuatilia habari husika ukilinganisha na vyombo vingine vya habari visivyopungua kumi…je vyanzo vyote vya habari husika vinasimamia habari hiyo hiyo kama ilivyo? Hapa namaanisha tusichukulie uzito wa habari katika chombo kimoja cha habari, hata kama ni chaguo lako…linganisha habari kwa kuunganisha matukio…kwa msemo maarufu wa lugha ya Malkia wanasema “connecting dots”
Kuwa na mashaka sana kuhusu habari iliyojenga “headline” ...vijana wa mjini hupendelea kuiita “habari ya mjini” kupitia chombo kimoja tu cha habari! Wakati mwingine huwa ni uzushi tu au chombo hicho cha bahari kutaka kumchafua mtu au kikundi cha watu fulani, au kuuza habari…Ichunguze habari hiyo kwa makini sana, Jielimishe Kwanza! ili ufahamu ukweli halisi wa mambo.
Nakutakia usomaji, utazamaji na usikivu mwema wa habari ukijiridhisha kuwepo kwa ukweli ndani yake.
Makala hii imetolewa na Jielimishe Kwanza! Social Enterprise kwa udhamini wa Ide@Spot na Enviro-Forum.
Habari /maulizo:jielimishekwanza@gmail.com

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni