inspire

inspire

Lebo

AFYA (8) AJIRA (5) BIASHARA (39) ELIMU (14) MAHUSIANO (2) MALEZI (16) MAZINGIRA (12) SAIKOLOJIA (48) VIJANA (7)

Business registration

Green Consulting

business consultancy

business consultancy

Business consulting-2

Business consulting-2

Professional Consulting

PDC

Swahili translator

Swahili translator

TANGAZO-KITABU

E-BOOK: MTAZAMO WAKO NI UPI?

TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- .... TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- ....

TANGAZO TUWEZESHANE

TANGAZO TUWEZESHANE

DARDY'S INVST-20/10/2017

DUNIA IKUONE

DUNIA IKUONE

Jumamosi, 25 Oktoba 2014

MTAZAMO: Wengine wamekosa kabisa…


Kuna wakati tunajiona na kujichukulia kama hatuna bahati, haki wala uwezo wa kumiliki vitu vya thamani, kusoma hadi ngazi za juu za elimu tuitakayo au kuwa na uhuru wa kipato kutuwezesha kutatua matatizo mengine ndani ya maisha yetu.Hii ni kwa sababu tunawaona wengine wakituzidi kimaisha kwa kumiliki vitu vya thamani na kusonga mbele kiuchumi ilihali hatujui wamepitia njia zipi kuvipata. Msemo ufuatao katika lugha ya Kiingereza unakazia...


Mwisho wa siku tunabaki kunung’unika, kulaumu wengine kwa wajibu wetu na hata kufikia hatua ya kumkufuru Mungu… “eti ana upendeleo” La hasha!
Tunasahau kuwa kwa vile au kile tulicho nacho, tukionacho kidogo kwa mtazamo wetu wa kibinadamu kuna wengine wamekosa kabisa na wanatamani wawe kama sisi. Je, ndugu msomaji unalitambua hilo? Pia una tambua kuwa kuna watu wengine hawajui walale wapi? na hawajui wale nini?... Haya ni maswali machache tu yanayoweza kututofautisha na wengine, na mwishowe kujiona tuna nafuu kuliko hao wengine.
Pia, ijulikane kuwa kuna watu ambao wanaombea kesho ifike salama, na wengine wanaomshukuru Mungu kwa uhakika wa pumzi tu! waipatayo kila siku ipitayo… kwa kifupi hawana uhakika wa maisha. Wengine ni wagonjwa wamelala vitandani kwa muda mrefu sasa…wanashauku kubwa ya kutembea na kufanya kazi tena.
Ndugu msomaji, kwa umakini kabisa naomba jichunguze, jilinganishe na wasio nacho na wenye shida utaona kuwa una nafuu kubwa kuliko hao wengine!
Ni sahihi kusema kuwa mwanadamu hatosheki na haridhiki kwa kile alicho nacho kwa wakati husika.Siku zote tunajitahidi kujiongeza, ndiyo maana matajiri hawachoki kutafuta pesa na mali…kila kukicha wanasaka pesa na kujilimbikizia mali, wakati huo huo watu wengine wakiwa hawaijui kesho yao.
Hali hii hukinzana kidogo na mtazamo wa mtaalam, mwanasaikolojia Maslow (1943, 1954) katika Maslow’s Hierarchy of needs” anasema; mwanadamu ana mahitaji yaliyoainishwa kwa ngazi 5 muhimu. Mwanadamu huamasika kufikia hitaji fulani…likitimia huitaji tena kufikia hitaji lingine, lingine na lingine. Inafikia wakati uhitaji wa mwanadamu “human needs” hufikia kikomo cha kujitosheleza kiasi cha kuweza kutoa msaada kwa wengine wasio nacho, hatua au ngazi hiyo ya juu namba 5, mtaalamu Maslow ameiita “self-actualization of human needs” … na ni nadra sana kufikia hatua hii kwa sababu ya vikwazo na kutotimiza mahitaji ya ngazi ya chini kama; hali ya kisaikolojia(1), usalama (2), uhusiano wa kijamii (3), na uwezo wa kujitambua na kujiamini(4).
Ngazi zote tano (5) ameziainisha kwa umbo la “pyramid”-umbo la nyumba za kihistoria za Wamisri, ukianzia ngazi ya chini (1) kwenda ngazi juu ya ukomo (5).
Katika hali isiyo ya kawaida, watu wanaoonekana wamefika kikomo cha uhitaji, wanaonekana kutoridhika na hali hiyo kiasi kwamba huendelea kuwanyonya kiuchumi wasio nacho.Nisiingie sana kiundani hapa kuwahusu hao waliofika hali ya kikomo cha uhitaji kama wanavyojiona. Sitaki kukuhamisha kwenye mada kuu…wengine wamekosa kabisa! Ila tuache kunung’unika, tulizike kwa kidogo tulicho nacho! ili kiwe chumvi ya hamasa katika kuelekea mafanikio makubwa tutakayo kuwa nayo.
Waswahili wanasema ridhika na kidogo ulicho nacho, usitafute makuu usiyoyaweza kwa wakati husika! Kinyume na hapo utaingia tamaa bure ya kuiba, kudhurumu wengine, kukiuka maadili ya kazi na hata kufikia hatua ya kuua wengine kwa kutamani pesa na mali.Sina maana tubweteke, kukaa na kusubiri miujiza au kuacha kukaza buti kujinasua kihalali katika hali ngumu ya maisha…La!
Huu ni mtazamo tu wa Jielimishe Kwanza! …unaweza kukusaidia, usikate tamaa.
Imetolewa na
Jielimishe Kwanza! Social Enterprise.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni