inspire

inspire

Lebo

AFYA (8) AJIRA (5) BIASHARA (39) ELIMU (14) MAHUSIANO (2) MALEZI (16) MAZINGIRA (12) SAIKOLOJIA (48) VIJANA (7)

Business registration

Green Consulting

business consultancy

business consultancy

Business consulting-2

Business consulting-2

Professional Consulting

PDC

Swahili translator

Swahili translator

TANGAZO-KITABU

E-BOOK: MTAZAMO WAKO NI UPI?

TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- .... TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- ....

TANGAZO TUWEZESHANE

TANGAZO TUWEZESHANE

DARDY'S INVST-20/10/2017

DUNIA IKUONE

DUNIA IKUONE

Jumamosi, 30 Mei 2015

MAZINGIRA: KUELEKEA SIKU YA MAZINGIRA DUNIANI JUNI 5


Kama ilivyo ada kila mwaka, tarehe 5 Juni duniani kote tunaungana kwa sauti moja na kauli mbiu moja kuadhimisha siku hii muhimu kwa mustakabali wa maisha yetu; kwa kuzingatia kuhifadhi na kuitunza “nyumba” (mazingira) inayotutunza.
Siku hii muhimu duniani ilianzishwa katika Mkutano mkuu wa Umoja wa Mataifa (UN General Assembly) mwaka 1972.Hivi leo “Siku Ya Mazingira Duniani” inaendelea kuheshimiwa duniani pote pia kusimamiwa kikamilifu na Kitengo cha Umoja wa Mataifa cha Mazingira-United Nations Environment Program (UNEP).Tukiwa kama familia moja duniani, husindikizwa na kauli mbiu itolewayo kila mwaka kwa kuzingatia maoni ya wataalam na wadau wa Mazingira duniani.
Kwa bahati nzuri kauli mbiu ya mwaka huu isemayo“Seven Billion Dreams.One Planet.Consume With Care kwa tafsiri ya lugha ya Kiswahili-Ndoto bilioni saba. Sayari moja.Tumia kwa uangalifu inatukumbusha kutumia rasilimali tulizonazo kwa uangalifu ukizingatia kuwa kuna ongezeko la idadi ya watu duniani (bilioni 7 hadi sasa) wenye ndoto tofauti tofauti, mabadiliko ya tabia nchi na wakati huo huo rasilimali nyingi zilizopo si rejereshi; zinatumika na hazijirudii au kurudishwa tena.
Shirika hilo la Umoja wa mataifa linalohusika na Mazingira duniani (UNEP) limeweka angalizo kuu kuwa kutokana na mfumo wa maisha ya binadamu, na uhitaji wa rasilimali ambazo kwa kiasi fulani zinaelekea kutokidhi ongezeko la idadi ya watu duniani; kuna hatari kubwa kuwa kama hali itaendelea kama kawaida kwa kuangalia makisio ya ongezeko hilo la watu bilioni 9.6 ifikapo mwaka 2050 tutahitaji kuwa na sayari 3 ili kukidhi mahitaji yetu.Unashangaa! Ndiyo huko tunakoelekea na vizazi vyetu. Wengine naona wameanza kuangalia uwezekano wa kuishi kule kwenye sayari ya “Mars”.Mimi na wewe je? Natania tu…
Imefika wakati wa kuamka sasa, kila mtu kuchukua wajibu sasa, kufanya pale anapoweza kuhakikisha kuwa rasilimali zilizopo zinatumika kwa uangalifu mkubwa kwa kuzingatia maendeleo endelevu- maendeleo yanayokumbuka na kuchukua taadhali kubwa kuwa kuna vizazi vijavyo vitakavyohitaji rasilimali zilizopo sasa.Ni maendeleo yanayozingatia manufaa ya jamii, mazingira yenyewe na uchumi kwa ujumla wake.Maendeleo yanayosahau kimoja kati ya hivyo vitatu, si maendeleo endelevu; yanapaswa kukosolewa, kubezwa na kuzomewa kwa kelele nyingi.Anza sasa!
Imetayarishwa na
Mwandishi wa Kitabu-“Mtazamo Wako Ni Upi?”
Imetolewa na
Jielimishe Kwanza!

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni