inspire

inspire

Lebo

AFYA (8) AJIRA (5) BIASHARA (39) ELIMU (14) MAHUSIANO (2) MALEZI (16) MAZINGIRA (12) SAIKOLOJIA (48) VIJANA (7)

Business registration

Green Consulting

business consultancy

business consultancy

Business consulting-2

Business consulting-2

Professional Consulting

PDC

Swahili translator

Swahili translator

TANGAZO-KITABU

E-BOOK: MTAZAMO WAKO NI UPI?

TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- .... TANGAZO:Kitabu kipya. Kitabu! Kitabu!Kinauzwa Katika Maduka Ya Vitabu.Pia M-Pesa 0754 572 143, Tigo Pesa 0716 075 826.Ili Kikufikie Ulipo, Tafadhali Ongezea Sh.10,000/- ....

TANGAZO TUWEZESHANE

TANGAZO TUWEZESHANE

DARDY'S INVST-20/10/2017

DUNIA IKUONE

DUNIA IKUONE

Jumamosi, 6 Julai 2013

MAZINGIRA: JUHUDI ZA WIZARA YA MALIASILI NA UTALII ZA KUANGAMIZA KUNGURU WEUSI TANZANIA



Kunguru mweusi-Corvus splendens(Picha nawww.tanzaniabirds.net)
Kwa kipindi kirefu kunguru weusi ambao Kibailojia hujulikana kwa jina Corvus splendens wamekuwa ni kero kwa maisha ya binadamu ikiwa ni ndege wanaomtegemea binadamu kwa kula mabaki ya vyakula vinavyotupwa ovyo,vifaranga vya kuku,bata na wanyama wengine wadogo wafugwao na ndio maana hujulikana kwa jina la Kiingereza “Indian House Crow” asili yao kutoka nchi za Kusini-Mashariki ya Asia katika nchi za China,Cambodia,Thailand,India na Sri-Lanka.



Kunguru weusi wana sifa zifuatazo: wana akili sana kiasi kwamba wanatambua mitego na silaha za moto,wanashambulia kwa pamoja wakiwa kwenye kundi, wana uwezo wa kuhakikisha kuwa wanapata vyanzo vya chakula.


Sifa nyingine ni kama:hawamwogopi binadamu, wanategemea makazi yao jirani na makazi ya binadamu,wanazaliana kwa kasi sehemu yoyote yenye idadi kubwa ya watu, ni wakorofi,wenye kelele na ushindani wa hali ya juu katika suala zima la kupata chakula.
(http://nitawriter.wordpress.com/2009/05/25/the-indian-house-crow-should-not-thrive/).


Ndege hawa waliletwa na Serikali ya Uingereza katika visiwa vya Zanzibar mwaka 1890 kwa lengo la kusafisha Mji mkongwe kutokana na ongezeko la uchafu.


Mnamo mwaka 1950-1955 kunguru weusi walifika Pwani ya Dar -es -salaam kwa njia ya majahazi na meli na kusambaa katika mikoa mingine kama vile Pwani,Lindi,Morogoro,Tanga na Mtwara.


Kutokana na kero kubwa kwa maisha ya binadamu,Wizara ya maliasili na utalii nchini Tanzania imeazimia kuwangamiza kunguru weusi kutokana na sababu zilizo sambamba na kero hizo;

·      Wanaeneza vimelea vya magonjwa mbali mbali kwa binadamu na kuku ikiwa ni pamoja na homa ya matumbo(Typhoid),kipindupindu na mdondo(Newcastle disease)

·  Wamekuwa na madhara na tishio kubwa kiikolojia kwa kuharibu viota,kula mayai na makinda ya ndege wengine wa asili na wanyama jamii ya mijusi

·      Huaribu miundo mbinu kama vile nyaya za umeme,simu na antenna za runinga

·      Kero kubwa kwa wakazi wa sehemu mbali mbali ikiwa ni pamoja na tabia yao ya kudokoa vyakula

·  Wamekuwa na tabia ya kutawanya uchafu uliokusanywa mahala pamoja, hivyo kuchafua mazingira



Serikali ya Tanzania ikishirkiana na Balozi za Denmark,Finland na USAID imeamua kuchukua juhudi za makusudi za kuwaangamiza ndege hao kwa kutumia mitego na sumu aina ya DRC 1339.Utekelezaji wa mradi huu ni wa miaka mitatu kuanzia Mwezi Novemba 2010 na kutarajiwa kukamilika Mwezi Desemba 2013.
Huu ni mtego maalumu unatumika kuwanasa kunguru weusi pekee (Picha na www.elitenetzwerk.bayern.de )
--> -->
Wizara ya Maliasili na Utalii inakumbana na changamoto zifuatazo katika zoezi zima la kuwateketeza kunguru weusi:

·      Gharama kubwa kwa ajili ya kununulia sumu DRC 1339 ambayo kwa kilo moja ni dola za Kimarekani 2500.

·      Kukithiri kwa uchafu hasa katika madampo yaliyowekwa kiholela mitaani ambayo ni chanzo kikuu cha chakula kwa kunguru weusi

·      Kunguru weusi hujifunza vyanzo vya kifo kwa haraka hasa pale wanapouawa kwa kutumia sumu na mizoga kutokusanywa mapema

·      Ni vigumu kupata idadi kamili ya kunguru weusi wanaouawa kwa kutumia sumu.

·      Uharibifu wa mitego unaofanywa na wananchi katika baadhi ya maeneo.

·      Kasi kubwa ya kusambaa kwa kunguru weusi hususan katika miji ya Pwani ya Bahari ya Hindi.

Kama ilivyoelezwa kuwa kunguru weusi hupendelea uchafu unaombatana na mabaki ya vyakula ili kuishi na kuzaliana. Kunguru weusi kama viumbe hai wengine wana tabia ya kuzaliana kwa wingi katika uwepo mkubwa wa chakula.

Tukishirikiana kuhifadhi taka za mabaki ya vyakula katika vifaa vilivyofunikwa vizuri na kutupa kwenye madampo yaliyo mbali na makazi inaweza ikawa njia mojawapo ya kupunguza idadi yao.


Makala hii imeandikwa kwa Kushirikiana na Kijarida cha Wizara ya Maliasili na Utalii-Tanzania kilichotolewa kwenye maonyesho ya Biashara(Saba Saba) mwaka 2013 na tovuti ya http://nitawriter.wordpress.com/2009/05/25/the-indian-house-crow-should-not-thrive/.

Imetolewa na
Jielimishe Kwanza!

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni